Sengerema FM

Sengerema kuzindua Sekondari mpya 11 mwakani

24 July 2024, 5:23 pm

Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Sengerema Binuru Shekidele akisalimiana na mwanafunzi.Picha na Richard Bogolele

Halmashauri ya Sengerema inatarajia kukamilisha ujenzi wa shule 11 mwakani na kuwa na jumla ya shule za Sekondari 46 waipongeza serikali ya awamu ya Sita

Na:Elisha Magege

Shule 11 mpya za Sekondari zinatarajiwa kukamilika mwezi Agosti mwaka huu na kuanza kutumika Januari 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.

Majengo ya shule mpya ya Sekondari inayojengwa katika halmashauri ya Sengerema.Picha na Richard Bagolele

Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hizo pamoja na ukarabati wa baadhi ya shule za msingi ,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Binuru Shekidele amesema kukamilika kwa shule hizo kutasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani sambamba na kupunguza kutembea umbali na utoro kwa wanafunzi.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Sengerema Binuru Mussa Shekidele akizungumzia ziara ya ukaguzi shule mpya

Aidha Shekidele amemshukuru Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassani kwa kuendelea kuleta fedha za miradi ya elimu kwa wananchi wa Halmashauri ya Sengerema.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Sengerema Binuru Mussa Shekidele akimpongeza rais Dr.Samia

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa Sekondari mpya ya Sogoso iliyopo kata ya Sima, na Igaka kata ya Buzilasoga ambazo zinatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2024 shule zingine mpya za Sekondari ambazo zinaendelea kukamilishwa ni pamoja na Igulumuki, Isole, Chamabanda, Busulwangili, Kagunga, Nyitundu, Balatogwa, Kabusuri na Ilekanilo ambazo zinajengwa kwa fedha za Serikali kuu na baadhi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania na kukamilika kwa shule hizi kutaifanya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuwa na shule 46 za Sekondari.