Sengerema FM

Waziri Nape aitaka jamii kutumia vizuri mitandao

18 July 2024, 8:07 pm

Waziri wa Habari,Mawasiliano na teknolojia Nape Nauye na viongozi pamoja na baadhi yya wananchi katika mnara wa mawasiliano ya Simu kisiwani Lyakanyasi. Picha na Elisha Magege

Mkoa wa Mwanza inajengwa minara 50 ya mawasiliano na mfuko wa mawasiliano kwa wote UCSAF itayowanufaisha zaidi ya wakazi 885,420 wa vijijini.

Na: Elisha Magege

Waziri wa Habari Mawasiliano na teknolojia Nape Nauye amewataka wazazi na walezi nchini kuwafundisha vijana maadili ya kitanzania na si kuwaacha wajifunze kwenye mitandao ya kijamii.

Waziri Nape ameyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara wilayani Sengerema ambapo amesema nivyema wazazi wakawafundisha mila na desturi za kiafrika ili kuepukana na matukio ya udhalilishaji yanayotokea kwenye mitandao ya kijamii Duniani.

Sauti ya Waziri wa Habari Mawasiliano na teknolojia Nape Nauye akizungumzia maadili kwa vijana nchini

Katika hatua nyingine Waziri Nape amesema serikali ya Dr. Samia inajenga minara 750 nchii nzima ili kuwasaidia wananchi wa vijijini kupata huduma za mawasiliano.

Sauti ya Waziri wa Habari Mawasiliano na teknolojia Nape Nauye akizungumzia ujenzi wa minara ya mawasiliano nchini

Naye Mbunge wa Sengerema Mh. Hamis Tabasam amemshukuru waziri Nape kwa kufika huku akiomba wizara yake kuvisaidia baadhi ya vijiji vilivyopo Sengerema, ambavyo havina mitandao ya mawasiliiano ya uhakika.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Sengerema Mh. Hamis Tabasam akizungumzia maeneo yenye changamoto ya mtandao

Waziri Nape amefanya ziara ya kikazi mkoa wa Mwanza katika wilaya ya Sengerema yenye lengo la kufuatilia upatikanaji wa mawasiliano vijijini na kutembelea mnara wa simu uliojengwa kwa ubia na serkali katika kisiwa cha Lyakanyasi Kata ya Chifunfu wilayani Sengerema.