Sengerema FM

Watakaotumia vyandarua kufugia vifaranga, bustani kukiona

10 July 2024, 3:00 pm

Afsa kutoka wizara ya Afya kitengo cha kudhibiti Malaria Bwn.Peter Gitanya akimkabidhi chandarua chenye dawa mama mkazi wa Sengerema.Picha na Halmashauri ya Sengerema

Mkoa wa Mwanza umepokea vyandarua Milioni 1.4 kwenda  Halmashauri 6 vitagawiwa kwa wananchi bila malipo zikilenga kaya zote ambazo zinakabiliwa na changamoto ya ugonjwa Maralia 

Na:Elisha Magege

Katika jitihada za kupambana na ugonjwa wa maralia nchini Halmashauri ya Sengerema inatarajia kungawa bure vyandarua vyenye dawa zaidi ya laki 2.

Mratibu wa maralia Halmashauri ya Sengerema Bwn. Abdurahman Mgonja akizungumzia zoezi la kugawa vyandarua vyenye dawa:Picha na Elisha Magege

Hayo yamesemwa na Bwn. Abdurahman Mgonja mratibu wa malaria Sengerema ambapo ameitaka jamii kutumia vyandarua hivyo katika matumizi sahihi yaliyokusudiwa na serikali kwa kutoa vyandarua hivyo.

Sauti ya Mratibu wa Maralia Bwn. Abdurahman Mgonja akizungumzia zoezi la ugawaji vyandarua vyenye dawa

Katika hatua nyingine mgonja amesema jamii imekuwa na dhana potofu kuwa vyandarua vyenye dawa vinavyotolewa na Serkali husababisha madhara kwa watumiaji ikiwepo kueneza kunguni na kupunguza nguvu za kiume kwa akina baba jambo ambalo siyo kweli.

Sauti ya mratibu wa Maralia Bwn. Abdurahman Mgonja akizungumzia kuhusu dhana potofu kuhusu vyandarua vyenye dawa

Aidha Mgonja amesema serkali haitasita kuwachukulia hatua wale watakao tumia vyandarua hivyo kufugia kuku au kwenye bustani za bongabonga.