Sengerema FM

Watoto waitaka serkali kukomesha ukatili unaoendelea nchini

17 June 2024, 7:28 am

Mandamano ya amani ya watoto katika maadhimisho ya siku ya mtoto Afrika Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye

Chimbuko la Maadhimisho haya ni Azimio lililopitishwa na uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) mwaka 1990 kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini waliouawa tarehe 16 Juni, 1976 kutokana na ubaguzi wa rangi.

Na:Emmanuel Twimanye

Watoto Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza wameiomba Serikali kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya watoto  vinavyoendelea  kushika kasi wilayani humo.

Hayo yamesemwa na watoto katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani  yaliyofanyika katika shule ya Sekondari Mwabaluhi wakati wakisoma risala  kwa mgeni rasmi  na kusema kuwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto bado vinaendelea ikiwemo  ubakaji ,ulawiti,ndoa za utotoni  na utumikishwaji katika ajira hatarishi hali inayopelekea kukatisha ndoto zao za kielimu.

Sauti ya watoto wakizungumzia siku ya mtoto Afrika

Afisa maendeleo ya jamii  katika Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema  Yuster Mwambembe  amewaomba watoto kutofumbia macho vitendo vya ukatili badala yake waendelee kuwafichua wanaowafanyia ukatili ili  wachukuliwe  hatua kali za kisheria.

Sauti ya Afisa maendeleo ya jamii Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema  Yuster Mwambembe

Naye katibu tawala wa Wilaya ya Sengerema  Cathbeth Midala  ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amewataka wazazi na walezi kutimiza jukumu la malezi kwa watoto ikiwa ni pamoja na kutimiza  mahitaji yao ya msingi ili kufikia ndoto zao za kielimu.

Sauti ya katibu tawala wa Wilaya ya Sengerema  Cathbeth Midala

Aidha kauli mbiu ya maadhimisho ya mtoto wa afrika kwa mwaka huu ni ‘’Elimu Jumuishi kwa watoto izingatie maarifa, maadili na stadi za kazi.