Sengerema FM

Moto wazuka na kuteketeza vitanda, magodoro Sengerema

21 May 2024, 7:49 pm

Picha ni baadhi ya vitu vilivyoteketea kwa Moto ndani ya Nyumba eneo la Tabaruka Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye

Matukio ya moto  yameendelea kushika kasi katika Kata ya Tabaruka ambapo kwa siku za hivi karibuni bweni la wanafunzi wa kike shule ya sekondari Tamabu liliteketea kwa moto mara mbili huku chanzo cha tukio hilo kikiwa hakijafahamika mpaka sasa.

Na: Emmanuel Twimanye

Moto  umezuka  ghafla  na kuteketeza vitu mbambali ikiwemo magodoro na vitanda katika nyumba ya mkazi mmoja wa kijiji cha Nyakato kata ya Tabaruka  wilayani Sengerema  mkoani Mwanza.

Akizungumzia tukio hilo mmiliki wa nyumba hiyo Paschal Kanyashi  amesema kuwa  wakati wanafamilia wote  wakiwa nje moto huo  ulizuka ghafla  ndani ya nyumba hiyo  na   kuteketeza   magodoro ,vitanda na nguo za wanafunzi.

Sauti ya Bwn.Paschal Kanyashi  Mumiliki wa Nyumba iliyoungua moto Tabaruka

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamesikitishwa na tukio hilo na kueleza kuwa mara baada ya kutokea moto huo walifanikiwa kuuzima.

Sauti za Wananchi mashuhuda wa Tukio la moto Tabaruka

Mwenyekiti wa Kitingoji cha Nyakato Senta  Deus Mabula  amethibitisha  kutokea kwa tukio hilo  na kuwashukuru wananachi kwa kushirikiana  kuzima moto huo .  

Sauti ya mwenyekiti wa Kitingoji cha Nyakato Senta  Deus Mabula 

Diwani wa kata ya Tabaruka Mh,Sospeter Busumabu  ameliomba Jeshi la zima moto kufanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto huo na kwamba  endapo   mtu yeyote  atakayebainika kuhusika katika  tukio hilo hatua kali zichukuliwe dhidi yake .

Sauti ya diwani wa kata ya Tabaruka Mh,Sospeter Busumabu 

Mkuu wa Jeshi la Zima moto Wilayani Sengerema  Juma Ngwembe  amewataka wananchi kuachana na matumizi ya mishumaa na vibatari  badala yake watumie nishati  ya jua ,taa za kisasa  na umeme ili kukabiliana na matukio hayo ya moto. 

Sauti ya Mkuu wa Jeshi la Zima moto Wilayani Sengerema  Juma Ngwembe