Sengerema FM
Sengerema FM
27 March 2026, 6:58 pm

Kutokana na kuanzishwa kwa mgodi wa dhahabu Wilayani Sengerema, Kampuni ya Sotta mining imetoa mafunzo kwa wafanyabiashara ili kuzijua na kuzitumia fursa zilizopo mgodini
Na,Emmanuel Twimnye
Wafanyabiashara Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza wameipongeza kampuni ya mgodi wa Sotta kwa kuwapatia mafunzo ya namna ya kuchangamkia fursa zitakazotokana na shughuli za mgodini, ikiwemo utaratibu wa kupata zabuni.
Wafanyabiashara hao wametoa pongezi hizo baada ya kupatiwa mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Sengerema ambapo wamesema kuwa wameelewa fursa zilizopo mgodini na namna ya kushiriki katika utoaji wa huduma na bidhaa, huku wakiahidi kuzitumia fursa hizo kujikwamua kiuchumi.
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wamepongeza hatua hiyo hatua hiyo itasaidia kukuza biashara na kuchochea uchumi wa wilaya kwa ujumla.
Mbunge wa Jimbo la Sengerema, Mh,Hamis Tabasam, amewahimiza wafanyabiashara kutumia vyema maarifa waliyopata ili wanufaike na fursa za uwekezaji wa mgodi huo.
Kwa upande wake, Mhandisi mkuu wa kampuni ya mgodi wa Sotta, Richard Ojendo, amesema ujenzi wa mgodi unaendelea na unatarajiwa kuanza uzalishaji rasmi mwaka 2027.