Sengerema FM

Madiwani Sengerema watakiwa kutanguliza mbele maslahi ya Wananchi

5 December 2025, 5:21 pm

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Senyi Ngaga akizungumza kwa madiwani Halmashauri ya Buchosa.Picha na Emmanuel Twimanye

Madiwani Halmashauri ya Sengerema wamekula kiapo cha kuwatukia wananchi wa Halmashauri hiyo baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oct.29 2025

Na,Emmanuel Twimanye

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza wamewatakiwa kwenda kufanya kazi kwa kutanguliza mbele maslahi ya wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh,Senyi Ngaga katika mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika katika ukumbi wa ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo uliokwenda sambamba na zoezi la kuapisha madiwani.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh,Senyi Ngaga

Awali wakiapishwa madiwani na Hakimu mfawidhi ya mahakama ya Wilaya ya Sengerema  Evoid Kisoka wameapa kuitumikia  Halmshauri ya wilaya ya Sengerema ,kulinda na kuitetea katika ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Madiwani wa Halmashauri ya Sengerema wakila kiapo.Picha na Emmanuel Twimanye
Sauti za Madiwani Halmashauri ya Sengerema wakila kiapo


Katika kikao hicho, baraza hilo limemchagua Diwani wa kata ya Nyamatongo Yanga Makaga  amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Halmshauri hiyo kwa kura 35 pamoja na makamu mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Diwani wa kata ya Kahumulo Fortunatus Nzwagi kwa kura 35 ambapo matokeo hayo yametangazwa na katibu tawala wa wilaya ya Sengerema Cathbeth Midala.

Sauti ya katibu tawala wa wilaya ya Sengerema Cathbeth Midala

Kwa upande wake Rose Mgasha kutoka Sekeretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kanda ya ziwa Mwanza,amewaomba madiwani kwenda  kufanya kazi kwa uadilifu .

Sauti ya Rose Mgasha kutoka Sekeretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kanda ya ziwa

Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema  Binuru Shekidele amewaomba madiwani kuungana na kwenda kuwatumikia wananchi .   

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Sengerema Binuru M. Shekidele akizungumza kwa madiwani Halmashauri hiyo.Picha na Emmanuel Twimanye
Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema  Binuru Shekidele

Naye Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema Yanga Makaga amewashukuru madiwani kwa kuwamini na kumchagua ili awatumikie huku akiagiza Halmashauri hiyo kuhakikisha inaongeza mapato pamoja na kupunguza matumizi ya fedha yasiyokuwa ya lazima.

Sauti ya Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema Yanga Makaga
Mwenyekiti Halmashauri ya Sengerema Yanga Makaga akizungumza na Madiwani.Picha na Emmanuel Twimanye