Sengerema FM

Watakiwa kumgeukia Mungu,badala ya kujitoa uhai

20 November 2025, 11:36 am

Picha ya kitanzi Picha na mitandao

Kwa mujibu wa taarifa zilizokusanywa na Radio Sengerema hivi karibuni matukio ya watu kujiua yanaonesha kuongezeko kwa kasi katika wilayani Sengerema.

Na.Emmanuel Twimanye

Wananchi Wilayani Sengerema mkoani Mwanza, wametakiwa kuwa na hofu ya Mungu na kuacha kuchukua maamuzi ya kujiua kwa kujinyonga, ili kukomesha ongezeko la matukio hayo katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Ustawi wa Jamii katika Kituo cha Afya Sengerema, Bi.Consolatha Magaka, kufuatia kukithiri kwa wimbi la matukio ya wananchi kujinyonga na kupoteza maisha wilayani humo .

Sauti ya afsa ustawi wa jamii wilayani Sengerema akizungumzia matukio ya kujiua watu

Katika hatua nyingine, Bi.Magaka  amewasihi  wanandoa kushirikishana watu wanaowaamini pindi wanapokumbana na changamoto za kifamilia, ili waweze kupata ushauri.  

Sauti ya afsa ustawi wa jamii wilayani Sengerema akizungumzia matukio ya kujiua watu

Baadhi ya wananchi, wamesema kinachopelekea wengi wao kushindwa kuweka wazi changamoto zinazowakabili ni  kukosekana kwa usiri miongoni mwa ndugu, jambo linalowafanya kubaki na matatizo kwa kuhofia kufichuliwa.

Sauti za baadhi ya wananchi mjini Sengerema wakizungumzia matukio ya watu kujiua

Matukio ya kujiua yameendelea kushamiri katika Wilaya ya Sengerema ambapo katika kipindi cha wiki moja pekee, jumla ya watu watatu   wamethibitishwa kupoteza maisha kutokana na kujitoa uhai.