Sengerema FM

Wasimamizi vituo vya kupigia kura watakiwa kuzingatia sheria

26 October 2025, 8:42 pm

Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Sengerema Ally Salim akifungua mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Picha na Mpiga picha wetu

Zaidi ya wasimamizi wakuu na wasaidizi wa vituo vya kupigia kura 1,950 wanatarajia kwenda kusimamia vituo 650 vya kupigia kura katika jimbo la Sengerema wamekura kiapo cha uadilifu ili kutekeleza jukumu la uchaguzi mkuu jimbo la Sengerema.

Na Mwandishi wetu

Wasimami wa  vituo vya kupigia kura  katika Jimbo la Sengerema Mkoani Mwanza wametakiwa kuzingatia kanuni ,miongozo  na sheria za uchaguzi ili uchaguzi huo ufanyike  kwa  uhuru  na  haki.

Kauli hiyo imetolewa na msimamizi wa uchaguzi  Jimbo la Sengerema Ally Salim wakati akifungua mafuzo ya siku mbili kwa wasimamizi wa vituo na wasimizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura  yaliyofanyika katika umbi wa shule ya sekondari Sengerema kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Rais,wabunge na madiwani .

Sauti ya msimamizi wa uchaguzi  Jimbo la Sengerema Ally Salim

Katika hatua nyingine   amewaomba  kujiepusha kuwa chanzo cha malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa kwa kushirikiana vyema na mawakala wa vyama hivyo watakaokuwepo kwenye vituo kwa mujibu wa sheria .

Sauti ya msimamizi wa uchaguzi  Jimbo la Sengerema Ally Salim

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameahidi kuzingatia kanunu ,miongozo na sheria za uchaguzi.

Sauti ya Baadhi ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura jimbo la Sengerema
Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura wakila kiapo. Picha na mpiga picha wetu