Sengerema FM

Wasimamizi wa uchaguzi kata watakiwa kufuata miongozo ya uchaguzi 2025

5 August 2025, 12:18 pm

Picha ni Hakimu mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Sengerema Evoid Kisoka. Picha na Emmanuel Twimanye

Ikiwa vyama vya siasa nchini vinaendelea na zoezi la kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali ikiwemo Udiwani,Ubunge na Urais Tume ya uchaguzi nayo inaendelea na zoezi la kuratibu wasimamizi wa uchaguzi nganzi za Kata na Jimbo.

Na;Emmanuel Twimanye

Wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Kata Jimbo la Sengerema Mkoani Mwanza wametakiwa kuzingatia taratibu ,kanuni ,sheria na miongozo ya uchaguzi  ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uhuru ,haki na amani.

Kauli hiyo imetolewa na Hakimu mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Sengerema Evoid Kisoka wakati akifungua mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari Sengerema yaliyokwenda sambamba na zoezi la kuwapisha wasimizi hao .

Sauti ya Hakimu mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Sengerema Evoid Kisoka

Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Sengerema  Ally Salim amesema kuwa idadi ya washiriki wa mafunzo hayo  yatakayodumu kwa muda wa siku tatu ni  52 kutoka katika kata 26 za  Jimbo hilo huku akiwaomba kuzingatia mafunzo hayo.

Sauti ya Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Sengerema  Ally Salim

Baadhi ya washiriki wa mafunzo  wamesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia  kusimamia  uchaguzi  kwa  weledi ikiwa ni pamoja na kuzingatia taratibu ,kanuni  ,sheria na miongozo  ili ufanyike kwa utulivu na amani.

Sauti za baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya kata

Aidha uchaguzi mkuu  wa wabunge ,madiwani na Rais unatarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu nchini.

Picha ni wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya kata wakila kiapo.Picha na Emmanuel Twimanye