Sengerema FM

Serikali,Under the same sun kuendelea kupinga ukatili dhiidi ya wenye ualbino

30 July 2025, 10:05 am

Picha ya pamoja kwenye mnala wa nithamini viongozi wa shirika Under the same sun. Picha na emmanuel Twiamanye

Shirika la Under the Same sun kwa kushirikiana na tasisi ya Village of Hop (VOH) wamefanya kumbukizi ya kuwakumbuka watu wenye ualbino waliouawa na kukatwa viungo vyao nchini, tukio hilo limefanyika mjini Sengerema kwenye mnala wa nithamini ulio na majina ya wahanga wa matukio hayo.

Na,Emmanuel Twimanye

Serikali Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza imeahidi kuendelea kuimarisha ulinzi dhidi ya watu wenye ualbino  ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria watu watakaobainika kujihusisha na mauaji dhidi yao  

Picha ya mkuu wa wilaya ya Sengerema Bi. Senyi Ngaga akizungumza na watu wenye ualbino.Picha na Emmanuel Twimanye

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh,Senyi Ngaga katika kumbukizi ya kuwaenzi watu wenye ualbino waliouawa ,kujeruhiwa pamoja na makaburi yao kufukuliwa  kufukuliwa Wilayani Sengerema.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Sengerema Senyi Ngaga akizungumzia ulinzi kwa albino Sengerema

Baadhi ya watu wenye ualbino wakiwemo waliowahi kushambuliwa wameiomba serikali kuendelea kuimarisha ulinzi dhidi yao.

Sauti ya baadhi ya watu wenye ualbino

Makamu mwenyekiti wa chama cha watu wenye ualbino Taifa  Alfred Kapole  ameiomba jamii kuhakikisha kila mmoja anakuwa balozi wa kupinga mauaji dhidi kundi hilo .

Sauti ya makamu mwenyekiti wa chama cha watu wenye ualbino Taifa  Alfred Kapole

Rais na mwazilishi wa Shirika la Under the Same Sun  kutoka nchini Canada Peter Ash amesema kuwa ndoto yake ni kuona siku moja watu wenye ualbino nchini Tanzania na kote  barani Afrika wanachukua nafasi yao stahiki katika kila ngazi ya jamii na kwamba siku za ubaguzi  dhidi ya watu wenye ualbino zitakuwa kumbukumbu iliyofifia.

Sauti ya Rais wa Shirika la Under the Same Sun  kutoka nchini Canada Peter Ash
Picha na Rais wa shirika la Under the same sun Peter Ash akizungumza na wananchi mjini Sengerema pamoja na watu wenye ualbino.Picha na Emmanuel Twimanye
Picha mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Sengerema Binuru M. Shekidere.Picha na Emmanuel Twimanye