Sengerema FM

Akamatwa akiiba koki na mita za maji mjini Sengerema

14 June 2025, 4:22 pm

Mtoto aliye kamatwa kwa wizi wa koki na mita za maji mjini Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye

Wimbi la wizi wa koki na mita za maji mjini Sengerema limezidi kushika kasi ambapo baadhi ya wezi wamekuwa wakidai kuiba na kuuza kama vyuma chakavu.

Na Emmanuel Twimanye

Mtoto mwenye umri wa miaka 15 katika mtaa wa Busisi Road  wilayani Sengerema Mkoani mwanza  amekamatwa   kwa  tuhuma za wizi wa mita na koki za maji.

Akizungumzia tukio hilo mtoto huyo akiwa chini ya ulinzi wa  uongozi wa  mtaa huo  amekiri kuiba mita na koki za maji na kueleza kuwa hiyo ni mara yake ya pili.

Sauti ya mtoto aliyekamatwa kwa wizi

Baadhi ya wananchi wamesema kuwa wizi wa mita na koki za  maji umekithiri katika mtaa huo na kuiomba serikali kuchukulia hatua kali za kisheria mtoto huyo aliyekamatwa ili liwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia hiyo.

Sauti za baadhi ya wananchi mjini Sengerema

Mwenyekiti wa mtaa wa Busisi Road Agnes Masai amethibitisha kukamatwa kwa mtoto huyo na kumpekeka katika kituo cha Polisi Wilayani Sengerema kwa hatua zaidi za kisheria.

Sauti ya Mwenyekiti mtaa wa Busisi road Bi.Agnes Masai