Sengerema FM

Tabasamu akabidhi mil.10 kwa bodaboda Sengerema

14 June 2025, 10:19 am

Mbunge wa jimbo la Sengerema Hamisi Tabasam akizungumza na waendesha pikipiki(Bodaboda) mjini Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye

Mai 19 waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Kassimu Majaliwa alikuwa na ziara wilayani Sengerema ya kukagua miradi na kusikiliza kero za wananchi ambapo bodaboda waliiomba serikali kuwasaidia fedha ili kutimiza malengo yao ya kununua koster kwa ajili ya usafirishaji,ambapo waziri mkuu aliahidi kuwachangia mil.10,na mbunge akaahidi mil 10 na jumla ya Tsh. Mil 50 zilipatikana .

Na, Emmanuel Twimanye

Waendesha Pikipiki maarufu Bodaboda katika Jimbo la Sengerema Mkoani Mwanza wamesahauriwa  kuangalia namna ya kukata Bima ya afya pamoja na kuchukua mkopo wa Pikipiki ili kuachana na pikipiki za mikataba  inayowaumiza .

Ushauri huo umetolewa na mbunge wa Jimbo la Sengerema Mh,Hamis Tabasam  katika mkutano wake na wanachama wa umoja wa waendesha Pikipiki uliofanyika katika uwanja wa Tabasam Wilayani Sengerema .

Sauti ya mbunge wa Sengerema Hamisi Tabasamu

Baadhi ya waendesha Bodaboda wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mh,Hamis Tabasama kwa  kuendelea kutoa ushirikiano kwa umoja huo .

Sauti za baadhi ya viongozi wa bodaboda mjini Sengerema

Kwa upande wake Kaimu  mkuu wa usalama barabarani Wilayani Sengerema  Inspekta Norshid Mussa amewaomba waendesha vyombo vya moto kuendelea kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali .

Sauti ya kaimu DTO Sengerema Norshid Mussa

Aidha  Mh,Tabasam ametumia mkutano huo  kukabidhi  shilingi milioni 10 kwa umoja wa waendesha Pikipiki ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za  kikundi hicho  kwa ajili ya ununuzi wa magari mawili ya umoja huo .