Sengerema FM

Heche asisitiza No reform No elections akiwa Sengerema

12 May 2025, 7:57 pm

Makamu mwenyekiiti wa Chadema JJohn Heche akizungumza na wananchi mjini Sengerema.PPicha na Emmanuel Twimanye

Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema kinaendelea na oparesheni yake ya No reform No eleections,ambapo tayari imeshaanza kanda ya victoria yenye mikoa ya Kagera,Geita na Mwanza.

Na Emmanuel Twimanye

Makamu mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) bara John Heche amesema chama hicho kitaendelea kushikiria msimamo wake wa  kutoshiriki  uchaguzi mkuu  unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu endapo     hayatafanyika mabadiliko ya sheria za uchaguzi .

Heche ametoa kauli hiyo leo Mei 12 mwaka huu wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika stendi ya zamani ya mabasi Mjini Sengerema.

Sauti ya John Heche Makamu mwenyekiti Chadema akizungumza na wananchi Sengerema mjini
Wananchi mjini Sengerema wakiungana na makamu mwenyekiti wa Chadema John Heche.Picha na Emmanuel Twimanye

Baadhi ya wanachama na viongozi wa chama hicho waliaombatana na makamu mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) bara  wameahidi kuendelea  kushikiria msimamo huo hadi pale mabadiliko ya sheria za  uchaguzi yatakapofanyika.

Sauti ya Baadhi ya viongozi wa Chadema walioambatana na makamu mwenyekiti wa Chadema

Aidha   Makamu mwenyekiti chama cha Demokrasia na Maendeleo  (CHADEMA) bara  John Heche  anaendelea na ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa kwa ajili ya kuzungumzia kampeni ya chama hicho walioiita  No Reforms No election wakimaanisha bila mabadiliko hakuna uchaguzi .

Makamu mwenyekiti John Heche akisalimiana na viongozi wa Chadema jimbo la Sengerema Picha na Emmanuel Twimanye.