Sengerema FM

Wananchi watakiwa kujitokeza kuboresha taarifa zao daftari la mpiga kura

30 April 2025, 6:49 pm

Maafsa uandikishaji wakiapa kuajili ya kuanza kazi ya kuboresha daftari la mpiga kura Jimbo la Sengerema.Picha na Elisha Magege

Tume huru ya taifa ya uchaguzi (INEC) imetangaza siku saba za wananchi kuboresha taarifa za mpiga kura katika jimbo la Sengerema, mkoani Mwanza.

Na,Elisha Magege

Afsa mwandikishaji jimbo la Sengerema Binuru Mussa Shekidele amewataka maafsa uandikishaji wanaotarajia kwenda kuanza kuboresha taarifa za mpiga kura kuzingatia maadali na kanuni za uandikishaji.

Shekidele ameyasema hayo kwenye semina maalumu kwa ajili ya maafsa uandikishaji iliyofanyika katika ukumbi wa Sengerema Sekondari,ambapo amesema ni vizuri kufanya kazi kwa kuzingatia viapo walivyoapa na kuacha kujihusha na matendo Maovu kwa kipindi cha utekelezaji wa majukumu yao.

Sauti ya afsa uandikishaji jimbo la Sengerema Binuru Mussa Shekidele Akizungumzia zoezi la uboreshaji daftari la mpiga kura

Kwa upande wake afsa Mteknolojia msaidizi wa INEC Bi.Eddah Aswile Amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao, kwani baada ya zoezi hili hilitarudiwa Tena mpaka uchaguzi mkuu 2030.

Sauti ya afsa Mteknolojia msaidizi wa INEC Bi.Eddah Aswile akizungumzia zoezi la uboreshaji Sengerema

Aidha maafsa uandikishaji wamesema wapotayari kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa kwao huku wakiwataka wananchi kujitokeza Kwa wingi kuboresha taarifa zao kwenye daftari la mpiga kura.

Baadhi ya waandikishaji wasaidizi wakielezea namna watakavyo enda kufanya kazi yao

Zoezi la uboreshaji wa taarifa za mpiga kura katika halmashauri ya Sengerema linatarajia kuanza tar1/05 na litadumu kwa muda wa siku 7 hivyo kila mmoja anatakiwa kuboresha taarifa zake hasa waliohama maeneo, kupoteza au kuharibu kitambulisho cha awali.

Maafsa uandikishaji wasaidizi wakisaini mkataba wa kuanza kazi ya kuboresha Daftari la mpiga kura Sengerema.Picha na Elisha Magege