Sengerema FM

Watakiwa kumuenzi JPM kwa kuchapa kazi

17 March 2025, 5:22 pm

Mch.James Bukwimba na Sheikh wa wilaya ya Sengerema Ahmed Jah Wakizungumzia kumbukizi ya miaka 4 kifo cha JPM. Picha na Emmanuel Twimanye

Tanzania imeazimisha miaka minne tangu rais wa awamu ya Tano Dr. John Pombe Magufuli afariki Dunia,ambapo baadhi ya wananchi na viongozi wamesema wataendelea kumuenzi kiongozi huyo kwa uchapa kazi wake uliokuwa umetukuka kwani alifanikiwa pakubwa kurejesha nidhamu kazini.

Na,Emmanuel Twimanye

Watumishi wa  serikali Wilayani Sengerema Mkoani  Mwanza  wametakiwa kuendelea kumuenzi kwa vitendo Hayati Dkt John Pombe Magufuli kwa kuchapa kazi kwa bidii , kupinga  rushwa na kudumisha nidhamu kazini.

Hayo yamesemwa na Viongozi wa Dini Wilayani Sengerema wakati wakizungumza na Radio Sengerema Fm  kuhusiana na kumbukizi ya miaka minne ya kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Dkt John Pombe Magufuli.

Sauti za viongozi wa Dini wilayani Sengerema wakizungumzia kumbukizi ya JPM

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii  Wilayani Sengerema  Stephano  Mahozi  amesema kuwa  vitendo vya rushwa na kupungua kwa nidhamu ya watumishi kazini  vinaendelea kushika kasi kwa sasa tofauti na utawala wa hayati Dkt John  Pombe  Magufuli .

Sauti ya mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii  Wilayani Sengerema  Stephano  Mahozi  akizungumzia miaka 4 bila JPM

Nao baadhi ya wazee  wilayani humo wamesema kuwa   baadhi ya viongozi wa serikali  hawamuenzi  hayati Dkt Magufuli kwa vitendo kutokana na kujihusisha na vitendo vya rushwa na kushuka kwa nidhamu kazini .

Sauti za wazee wilayani Sengerema wakizungumzia jamii inavyo muezi JPM

Aidha Hayati Dkt. John Pombe. Magufuli alizaliwa  Oktoba 29, 1959 Wilayani Chato   Mkoa wa Geita na kufariki Dunia  machi 17 mwaka  2021  kwa ugonjwa moyo .