Sengerema FM

SEUWASA yawadaka Walimu wakijiunganishia maji Kinyemela

20 February 2025, 4:59 pm

Meneja utawala na Rasilimali watu wa Mamlaka ya maji Mjini Sengerema Mussa Bujiku akizungumza na watuhumiwa wa wizi wa maji na viongozi wadamizi SEUWASA. Picha na Emmanuel Twiamanye

Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Sengerema (SEUWASA) Imekuwa ikijiendesha kwa hasara kwa muda mrefu jambo lililoibua maswali mengi kwa baadhi ya wananchi mjini hapo, ambapo tayali mamalaka imeanza kuchukua hatua kwa kufuatilia miundo mbinu yake.

Na,Emmanuel Twimanye

Walimu watatu  wamekamatwana mamlaka  ya maji safi na usafi wa mazingira Mjini Sengerema (SEUWASA)kwa tuhuma ya wizi wa maji Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.  

Meneja utawala na Rasilimali watu wa Mamlaka ya maji Mjini Sengerema Mussa Bujiku amethibitisha kukamatwa kwa  walimu hao watatu katika  oparesheni  iliyoendeshwa na mamlaka hiyo kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Sengerema huku akiwaonya wananachi kuaachana na wizi wa maji ili kuepuka kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Sauti ya Meneja utawala na Rasilimali watu wa Mamlaka ya maji Mjini Sengerema Mussa Bujiku

Wenyeviti wa serikali za mitaa ,mabalozi  pamoja na wananchi wamesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watumishi wa serikali kutuhumiwa kujihusisha na wizi wa maji na  kuomba vyombo vya dola kuwachukulia hatua kali za kisheria ili kukomesha vitendo hivyo.

Sauti ya baadhi ya viongozi wa mitaa na wananchi mjini Sengerema

Baadhi ya walimu  waliokamatwa   hawakuwa na sababu za msingi za kujieleza .

Sauti ya walimu waliojiunganishia maji kinyemela mjini Sengerema
Maofisa SEUWASA Wakifukua mabomba ya mtandao wa maji uliounganishwa kinyemelea