Sengerema FM

Moses akutwa na baiskeli aliyoiba kanisani Sengerema

6 October 2024, 5:21 pm

Kijana Moses Emmanuel Nyanda akiwa ameshikilia baiskeli aliyoiiba kanisani.Picha na Emmanuel Twimanye.

Jamii imekua haiwaamini vijana kutokana na kuwa na tamaa ya mali za haraka jambo lililopelekea kuwa wadokozi na wezi wa vitu mbalimbali kwenye maeneo yao.

Na;Emmanuel Twimanye

Kijana  mmoja mwenye umri wa miaka 17 amekamatwa na  Jeshi la Polisi jamii kata ya Misheni Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza wakati  akimuuzia Baiskeli mkazi wa kata hiyo aliyoiba katika kanisa la Parokia ya Yesu Kristo Mfalme Sengerema.

Akizungumzia tukio hilo akiwa chini ya ulinzi wa Polisi jamii kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Moses Emmanuel Nyanda  amekiri kuiba Baiskeli hiyo kanisani hapo na kwenda misheni kuiuza ndipo alipokamatwa na Jeshi la Polisi jamii.

Sauti ya kijana Moses Emmanuel Nyanda  anaye daiwa kuiba baikeli kanisani

Mmiliki wa Baiskeli hiyo Faustine  Chilimila amesema kuwa baada ya kumaliza misa ya kwanza    hakuikuta   baiskeli yake  alipokuwa ameiegesha na muda mfupi alipigiwa simu akitaarifiwa kuwa kijana mmoja amekamatwa misheni akiwa na Baiskeli hiyo. 

Sauti ya Bwn. Faustine  Chilimila mmiliki wa baiskeli iliyoibiwa kansani

Mkazi wa misheni aliyetaka kuuziwa Baiskeli hiyo Masumbuko Costantine  amesema kuwa  wakati anauziwa  Baiskeli na  kijana huyo  alimuomba kibali na kukosa ndipo alipomshtukia   na kutoa taraifa kwa jeshi la polisi jamii na kufanikiwa kukamatwa.

Sauti ya mkazi wa misheni mjini Sengerema aliyetaka kuuziwa baiskeli ya wizi Masumbuko Costantine

Baadhi ya wananachi wa kata hiyo wamesikitishwa na tukio hilo na kuwaomba vijana kuacha kujihusisha na vitendo vya wizi.

Sauti ya baadhi ya wananchi mjini Sengerema wakizungumzia wizi kwa vijana

Katibu wa Parokia ya Yesu  Kristo Mfalme Sengerema  Nichorous Chumus amekiri Baiskeli hiyo kuibiwa katika kanisa hilo na  kuwaomba wazazi kuwalea vijana katika maadili mema.

Sauti ya Nichorous Chumus Katibu wa Parokia ya Yesu  Kristo Mfalme Sengerema akikiri kuibiwa baiskeli kanisani hapo 

Naye Kamanda wa Polisii  jamii kata ya Misheni  Rajabu Tunge  amethibitisha kijana huyo kukamatwa na Jeshi hilo wakati akiuza Baiskeli hiyo na kuwaonya vijana kuacha kujihusisha na wizi.

Sauti ya Kamanda wa Polisii  jamii kata ya Misheni  Rajabu Tunge akizungumzia namna walivyomzibiti mwizi wa baiskeli