Sengerema FM

Wakatazwa kujihusisha na kilevi wakati wa uandikishaji

20 August 2024, 12:13 pm

Afisa mwandikishaji wa Jimbo la Sengerema Binuru Shekidele akizungumza na maafisa uandikishaji daftari la mpiga kura. Picha na Emmanuel Twimanye

Tume huru ya uchaguzi nchini inatarajia kuanza zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura kwa mikoa ya Mwanza na Shinyanga tar21/08/2024

Na:Emmanuel Twimanye

Maafisa uandikishaji  wa  uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura katika  Jimbo la Sengerema Mkoani  Mwanza    wametakiwa kuzingatia miiko na tarabibu za kazi ikiwemo  kutojihusiaha na  ulevi  sambamba na  kutumia lugha zizizokuwa na staha wakati wa uandikishaji ili kuepuka kuharibu zoezi hilo.

Kauli hiyo  imetolewa na  Afisa mwandikishaji wa Jimbo la Sengerema Binuru Shekidele wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya  uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika ukumbi wa mikutano wa shule ya Sengerema sekondari .

Sauti ya Afisa mwandikishaji wa Jimbo la Sengerema Binuru Shekidele

Katika hatua nyingine amewataka kutunza vifaa vitakavyotumika katika zoezi hilo  kwa kuwa  vimenunuliwa  kwa  gharamu kubwa.

Sauti ya Afisa mwandikishaji wa Jimbo la Sengerema Binuru Shekidele

Awali Afisa uchaguzi wa Tume huru ya uchaguzi Jimbo la Sengerema  Yusta Mwambembe  amesema kuwa mafunzo hayo yanashirikisha jumla ya washiriki  654  huku akiwapongeza kwa kuchaguliwa katika zoezi hilo. 

Sauti ya Afisa uchaguzi wa Tume huru ya uchaguzi Jimbo la Sengerema  Yusta Mwambembe

Nao washiriki wa mafunzo wameahidi kwenda kutekeleza  zoezi hilo kwa weledi baada ya kupatiwa  mafunzo hayo  . 

Sauti ya washiriki wa mafunzo ya uandikishaji wapiga kura

Aidha zoezi la  uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura katika  Jimbo la Sengerema  linatarajiwa kuanza  August 21  hadi  27 mwaka huu  likiwa na kauli mbiu   isemayo  “Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi  wa uchaguzi bora”