Sengerema FM

Afariki baada ya kujeruhiwa na kiboko akivua samaki ziwa Victoria

29 July 2024, 7:59 am

Picha ya kiboko akiwa majini.Picha na website ya TAWA

Matukio ya watu kujeruhiwa na wanyama wakali wanaoishi majini yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara kwa wakazi wanaoishi kadokando na kufanya kazi ndani ya Ziwa Victoria ambapo wamekuwa wakiiomba Serikali kupitiwa TAWA kuongeza juhudi za kuwawida wanyama hao hasa Kiboko na Mamba.

Na:Elisha Magege

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina Nyili Katerezi (4O) mkazi kanywengezi  kijiji cha Nyandago kata ya Butundwe  amefariki Dunia baada ya kujeruhiwa vibaya na mnyama aina ya kiboko wakati akiwa kwenye majukumu ya uvuvi katika mwalo wa Nyandago ndani ya ziwa Victoria.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Mwenyekiti wa kitongoji cha kanywengezi Bwn. Enos Makaranga Magoji amesema tukio hilo ni la pili kutokea kwenye kitogoji hicho huku akitoa tahadhali kwa wananchi wanao fanya shughuli zao kandokando ya ziwa kuwa makini na wanyama hao.

Sauti ya Mwenyekiti wa kitongoji cha kanywengezi Bwn. Enos Makaranga Magoji

Akizungumza kwa niaba ya familia Martini Mlengosha Amesema  wamepokea kwa masikitiko tukio la kujeruhiwa kwa ndugu yao  na mnyama aina kiboko na kupelekea kupoteza maisha huku wakiiomba serikali kupitia wizara ya maliasili kuweka mikakati thabiti kwa ajili ya kuwazuia wanyama hao ambao kwa maeneo yao ni mara kwa mara wanajitokeza.

Sauti ya msemaji wa familia iliyopata msiba

Kufuatia tukio hilo mbunge wa Jimbo la Busanda Mhandisi Tumaini Magesa na diwani wa kata hiyo Titos  Pamba  wamefika kutoa pole kwa familia na kuahidi kulipeka suala hilo kwa waziri mwenye damana husika.

Sauti ya mbunge wa jimbo la Busanda na viongozi

Nao baadhi ya wananchi kijiji hicho wameendelea kuiomba serikali kuliangalia suala hilo kwa umakini mkubwa matukio hayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara.

Sauti ya baadhi ya wananchi wakazi wa kijiji cha Nyandago

Aidha katika ajali hiyo iliyotokea majira ya saa kumi usiku chombo walichokuwa wanatumia kuvua walikuwepo watu watatu ambapo  wawili walinusirika na mmoja kujeruhiwa vibaya.