Orkonerei FM

CCM Simanjiro yaadhimisha miaka 49, yajivunia mafanikio

3 February 2026, 11:49 am

Na Dorcas Charles

Wakati CCM ikiazimisha miaka 49 tangu kuasisiwa kwake mwaka 1977, Katibu wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Ndg. Mbula Teresia Igembia, ameelezea mabadiliko makubwa ya kijamii na kiuchumi yaliyopatikana wilayani humo. Katibu amebainisha kuwa tangu kuzaliwa kwa chama hicho, kumekuwa na maboresho ya dhahiri katika sekta za afya, hususan afya ya mama na mtoto, ujenzi wa miundombinu ya shule, na barabara. Ameongeza kuwa utekelezaji wa ahadi za chama umewajengea wananchi imani kubwa, hali inayofanya CCM kuendelea kuwa kimbilio la wakazi wa Simanjiro katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Akizungumzia na na mwandishi wetu Dorcas Charles Bi. Igembya amesema kuwa changamoto za ardhi ambazo zimekuwa zikiwakabili wakulima na wafugaji, Katibu Igembia amesisitiza kuwa Ilani ya CCM imetoa mwelekeo madhubuti wa kutatua migogoro hiyo. Alibainisha kuwa tayari Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Ndg. Peter Toima, ametoa maelekezo mazito kwa makatibu na viongozi wa chama kuhakikisha migogoro ya ardhi inashughulikiwa kwa haki na weledi. Katibu alikemea baadhi ya viongozi wa vijiji wanaohusishwa na uuzaji holela wa ardhi, akisema kuwa mchakato wa kutatua changamoto hizo unaendelea kwa kasi ili kuleta amani ya kudumu kati ya makundi hayo ya uzalishaji.

Karibu kusikiliza mahojiano hayaa.