Orkonerei FM
Orkonerei FM
11 February 2025, 2:08 pm

Wadua wa afya African Afya Initiative, CACHA na halmashauri ya wilaya ya Simanjiro kwa pamoja wanashirikiana kutoa huduma za afya kwa magonjwa mbalimbali katika Kata za Terrat na Komolo wilayani Simanjiro.
Na Baraka David Ole Maika.
Akizungumza na Orkorenei Fm Radio mratibu wa Africa Afya Iniative na CACHA Bwana Steve Martin amesema kuwa Huduma hiyo inatolewa kwa watu wote katika Kata ya Terrat na Kata ya Komolo.
Aidha Bwana Steve Martin amebainisha ratiba ya utoaji wa huduma za Matibabu kwa siku zote katika kata hizo mbili ya terrat na komolo.
