Orkonerei FM

Kilimo cha umwagiliaji kinavyowawezesha wanawake Simanjiro

22 December 2025, 9:30 am

Afisa Mahusiano wa TACCEI (The Tanzania Conservation and Community Empowerment Initiative) Ndg. Yohhana Meliyo Mollel akiwa katika moja ya shamba la mwanamke aliyewezeshwa na taasisi hiyo.

Na Isack Dickson,

Katika Wilaya ya Simanjiro, mabadiliko ya tabianchi si hadithi tena, bali ni ukweli mchungu unaohatarisha usalama wa chakula, hata hivyo kundi la wanawake 111 katika vijiji 5 limeamua kubadili mwelekeo. Kupitia ushirikiano na shirika la TACCEI, wanawake hawa wamegeuza ardhi kame kuwa mashamba ya kijani kibichi kwa kutumia teknolojia rahisi ya umwagiliaji.

Bi Vaileth Kadogo akiwa ameshikilia mihogo iliyotoka katika shamba lake la kumwagilia kijijini kwake Loswaki.

Makala hii ya kusisimua inakupeleka Simanjiro kusikia simulizi ya Vaileth Kadogo na wenzake, ambao si tu wanatunza mazingira, bali wanatekeleza kwa vitendo malengo ya Agenda 2063 ya Afrika na SDG 5 kuhusu usawa wa kijinsia.

Moja ya vifaa vinavyotolewa na taasisi ya TACCEI kwa akinamama kwa ajili ya kumwagilia mashamba yao ni madumu haya ya mvua maalum.
Makala ya Sauti