Picha ikonesha shamba la Bwana Abraham Leposo mkaazi wa teraat kilimo cha umwagiliaji
Orkonerei FM

Kilimo cha Umwagiliaji: Suluhisho la Ukame na Njia ya Uhakika ya Kipato

28 November 2025, 9:14 am

Shamba la mmoja wa wakulima kwanjia ya umwagiliaji kata ya Terrat Wilaya ya Simanjiro Bwana Abraham Lengine Leposo, 21 Novemba 2025, ambapo analima aina tofautitofauti ya mazao ikiwamo mbogamboga,mahindi na miti ya Matunda,shamba hili linaukuwa wa hekari 6 na anatumia maji ya korongo la Terrat. (Picha na Evanda Barnaba).

KURUNZI MAALUMU

Katika hali ya ukame uliokolea na utegemezi wa mvua, hasa Manyara, Orkonerei FM inakuletea Kurunzi Maalumu inayoangazia Kilimo cha Umwagiliaji kama mkombozi mkuu. Sikiliza jinsi wakulima wa Kata ya Terrat, Simanjiro, wanavyotumia vyanzo vidogo vya maji kama korongo kufanya kilimo cha mboga mboga na mazao mengine mwaka mzima, wakijiongezea kipato na kuhakikisha familia zinapata chakula.

Kipindi hiki kinakuletea sauti za wakulima wadogo na wakubwa waliofanikiwa, Aliyekuwa Afisa Kilimo wa Kata anayeeleza umuhimu wa umwagiliaji kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na Diwani wa Terrat Jackson Matery akizungumzia mikakati ya miundombinu. Ni mwongozo kamili wa jinsi ya kugeuza changamoto ya ukame kuwa fursa ya mafanikio ya kiuchumi!

Kipindi kamili cha Kurunzi Mtangazaji mkuu Dorcas Charles.