Mwajuma Bakari Ally mtia nia wa nafasi ya ubunge jimbo la simanjiro 2025
Orkonerei FM

Vijana wa kike jamii ya wafugaji wanaingia kwenye siasa?

3 October 2025, 12:19 pm

Mtiania nafasi ya Ubunge Jimbo la Simanjiro Bi. Mwajuma Bakari Ally akinadi sera zake mbele ya wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi katika mchakato wa ndani Agosti 2025, akiwa ni Kijana wa kike pekee kati 6 waliopitishwa na chama chake. (Picha na Isack Dickson)

Na Dorcas Charles-Kurunzi Maalum

Idadi ndogo ya vijana wa kike kutoka jamii za kifugaji katika Wilaya ya Simanjiro wanaojitokeza kugombea nafasi za uongozi inazua maswali mengi juu ya ushiriki wa wanawake vijana katika siasa. Hali hii inajiri wakati nchi ikiendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Katika Kurunzi Maalum (Kipindi) kinachorushwa na Orkonerei FM Radio, kiliangazia changamoto na fursa zinazowakabili vijana hawa. Dorcas Charles, mtangazaji wa makala hii, alieleza kuwa vikwazo vikuu ni pamoja na mila na desturi za jamii, majukumu ya kifamilia na ukosefu wa elimu ya uraia.

Licha ya takwimu za mwaka 2020 kuonesha asilimia ndogo ya wanawake vijana waliojitokeza kugombea, bado kuna matumaini. Jamii na serikali zina jukumu la kuhakikisha vijana hawa wanapata fursa sawa na usawa wa kijinsia unaimarishwa katika michakato yote ya kidemokrasia.

Sikiliza kipindi kizima cha “Kurunzi” ili kupata maelezo zaidi juu ya mada hii muhimu.

Makala ya Kurunzi kuhusu umuhimu wa vijana, hasa wa kike, kushiriki kwenye uchaguzi na michakato ya kisiasa.