Orkonerei FM
Orkonerei FM
6 August 2025, 11:36 am

Na Isack Dickson
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Simanjiro, Ndugu Amos Shimba, ametangaza rasmi matokeo ya kura za maoni kwa nafasi ya Ubunge Jimbo la Simanjiro kupitia mahojiano maalum na Orkonerei FM Radio.
Kwa mujibu wa Katibu huyo, kura zilizotakiwa ni 16,823, na kura zilizopigwa ni 14,574, huku kura 141 zikiripotiwa kuwa zimeharibika.
Akizungumza na Orkonerei FM baada ya kutangaza matokeo, Ndugu Amos Shimba alisema kuwa hatua inayofuata ni utekelezaji wa mchakato wa vikao vya chama, vinavyohusisha:
“Chama kina utaratibu wake wa ndani wa kuchambua majina haya na kuwasilisha mapendekezo hadi kufikia uteuzi wa mwisho wa mgombea Ubunge. Wanachama wamefanya kazi yao, sasa tusubiri kwa utulivu hadi jina litakapotangazwa rasmi,” alisema Shimba.
Aidha, alitoa wito kwa wanachama na wapenzi wa CCM kuendelea kudumisha mshikamano akisema, “Umoja wetu ndiyo ushindi wetu. Simanjiro tunajipanga kuhakikisha kura nyingi zinakwenda kwa wagombea wa CCM, kuanzia kwa Rais Jemedari Dkt. Samia Suluhu Hassan hadi kwa Mbunge na Madiwani.”