Karagwe FM

Recent posts

27 April 2021, 12:02 pm

Timu ya Nyaishozi SC kutua Bungeni wiki hii

Na Shabani Ngarama, Karagwe FM Timu ya Nyaishozi kutoka wilaya ya Karagwe iliyowakilisha mkoa wa Kagera kwa kupanda daraja la pili katika michuano ya fainali ya ligi za mikoa iliyofanyika mkoani Lindi imepata fursa ya kupumzika Dodoma wakati ikitokea mkoani…

26 April 2021, 8:20 pm

Wakosa makazi kwasababu ya Mafuriko.

Mvua zinazoendelea kunyesha katika sehemu mbalimbali Wilayani Missenyi zimesababisha baadhi ya barabara za mitaa na makazi ya watu katika mji mdogo wa Kyaka Bunazi kujaa maji huku baadhi ya wakazi wa mji huo wakilazimika kuhama makazi Mkuu wa Wilaya Missenyi…

24 April 2021, 7:28 am

Halmashauri zote zapewa maagizo.

Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti amewataka wajasiriamali wadogo kuchangamkia fursa ya kupata vitambulisho vipya vya kielectroniki vilivyoanza kutolewa na mamlaka ya mapato Tanzania TRA. Ametoa wito huo wakati alipokuwa akiongea na wakuu wa wilaya pamoja na…

20 April 2021, 9:26 am

Jeshi la zimamoto laungana na Skauti kukabili moto.

Jeshi la zimamoto na uokoaji wilayani Karagwe limeungana na Skauti wilayani humo ili kuongeza nguvu katika kukabiliana na majanga ya moto ambayo yamekuwa yakiteketeza mali za watu na kuwarudisha nyuma kimaendeleo. Staff Sergeant Peter Mbale ni Kamanda wa Jeshi la…

19 April 2021, 4:32 pm

Sekondari 15 kati ya 22 zafanikisha Lishe

Afisa Elimu sekondari wilayani Missenyi mkoani Kagera Mwl Saverina Misinde amezipongeza shule za sekondari 15 za serikali zinazotoa huduma ya chakula cha mchana ili kuwawezesha wanafunzi kujifunza vizuri wakiwa wameshiba Pongezi hizo amezitoa hivi karibuni wakati Kamati ya fedha Utawala…

17 April 2021, 5:21 pm

Wananchi walia na ubovu wa Barabara.

Wananchi wa kitongoji cha Karundu kata ya Bugene wilaya ya Karagwe mkoani Kagera wameiomba Halmashauri ya wilaya Karagwe iwatengenezee barabara za kitongoji hicho kwani wao wamejitolea bila kupata msaada mpaka wamechoka. Wananchi hao wamebainisha kero hiyo wakiwa kwenye mkutano wa…

16 April 2021, 9:32 pm

Kitendawili chateguliwa Kyenjubu.

Wananchi walionunua viwanja eneo la Kyenjubu Missenyi Mkoani Kagera wako mbioni kukabidhiwa viwanja vyao ili waviendeleze Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Missenyi Innocent Mukandala amesema kuwa shughuli yakutengeneza barabara iliyokuwa imekwamisha zoezi lakukabidhi wananchi viwanja vyao inaendelea vizuri nakwamba…

16 April 2021, 9:14 pm

Sita wanusurika kifo baada ya kutokea ajali

Watu sita wakiwemo wanafunzi wanne wamenusurika kifo baada ya kutokea ajali ya gari lenye namba za usajili T 780 DNS iliyotokea eneo la mzunguko wa barabara ya Rwamishenye Manispaa ya Bukoba Mkoani kagera. Kamishina msaidizi wa Polisi na Kaimu kamanda…

KARAGWE FM PROFILE

UTANGULIZI.
Radio Karagwe ni Radio ya kijamii iliyoanzishwa na shirika lisilokuwa la kiserikali lijulikanalo kama Karagwe Media Association (KAMEA).Ilianza kurusha matangazo yake Desemba 11.2007 kupitia masafa ya 91.4 MHz kwa ufadhili wa shirika la nchini Denmark (ULD80 Karagwe Venor) waliowezesha mafunzo kwa watumishi na upatikanaji wa vifaa.

DIRA.
Kuziba pengo la mawasiliano kwa wananchi wa Karagwe ambao kwa wakati huo hawakuwa na uwezo wa kusikiliza radio za Tanzania kutokana na jiongrafia ya eneo.

MAENEO REDIO INAKOSIKIKA
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na ULD80 June mwaka 2012 Radio Karagwe ina zaidi ya wasikilizaji milioni 1.2.(KM 200 KUTOKA MAKAO MAKUU).Inasikika katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kagera,katika wilaya za Karagwe, Kyerwa, Missenyi, Muleba na Bukoba Vijijini. Inasikika katika maeneo machache wilaya za Ngara, Biharamulo na Bukoba manispaa. Pia inasikika maeneo ya nchi jirani za Uganda, Burundi na Rwanda.

MAWASILIANO.
S.L.P 316,KARAGWE KAGERA TZ
E-mail : radiokaragwe@gmail.com
Phone: +255 754 677 708 / +255 689 471 171