Orkonerei FM

Kumbukeni kujiandaa kukabiliana na ukame Terrat Simanjiro

15 May 2025, 3:03 pm

Ng’ombe akitembea juu ya ardhi kavu (Picha kwa msaada wa Mtandao)

“Huu ndiyo wakati wa kuhakikisha maeneo yetu ya malisho yanalindwa, kuhifadhi mbegu za majani, na kuhakikisha tunafuata utaratibu wa kulisha mifugo ili kipindi cha ukame kisitukute hatuna maandalizi,” Kone Medukenya

Na Baraka David Ole Maiaka

Jamii ya wafugaji wa kijiji cha Terrat, Wilaya ya Simanjiro, inakumbushwa kutumia vizuri msimu huu wa mvua kuandaa malisho kwa ajili ya mifugo ili kuepuka hasara katika kipindi kijacho cha kiangazi.

Mwaka uliopita wafugaji walipoteza mifugo yao huku wengine wakitumia gharama kubwa kunusuru mifugo kutokana na ukosefu wa malisho na maji. Mfugaji Daniel Leboi Ngoira anakumbusha uzoefu wake katika makala fupi.

Simulizi ya Baraka David Ole Maika