Karagwe FM

MNEC Karim Amri aunga mkono ligi ya Bashungwa kwa mipira 50

19 July 2024, 6:18 pm

Mjumbe wa wa halmashauri kuu ya CCM Taifa kutoka Kagera Karim Amri. Picha na Eliud Henry

Mbunge wa jimbo la Karagwe na waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa ameendeleza utamaduni wake wa kutoa burudani kwa vijana jimboni humo kupitia ligi ya mpira wa miguu maarufu kama “Bashungwa Karagwe Cup”

Na Shabani Ngarama

Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi CCM Taifa kutoka mkoa wa Kagera Karim Amri amemshukuru mbunge wa jimbo la Karagwe na waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa kwa kuanzisha ligi kwa vijana wilayani Karagwe kwa kuwa itasaidia kukuza vipaji na kuwawezesha vijana wengi kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu na uchaguzi mkuu mwaka ujao

Amesema hayo Julai 18, 2024 wakati akichangia mipira 20 kati ya 50 aliyoikusudia kwa ajili ya kuhakikisha ligi hiyo inafanikiwa kama ilivyopangwa na kuongeza kuwa Bashungwa ameanzisha ligi kwa wakati mwafaka ambapo kupitia kwa waratibu wa ligi na chama cha mapinduzi kinapata nafasi ya kuhamasisha vijana kwenda kujiandikisha kwenye daftrai la kudumu la mpiga kura

Sauti ya mjumbe wa wa halmashauri kuu ya CCM Taifa kutoka Kagera bw. Karim Amri
Karim Amri akiwa na viongozi wengine wakati wa kukabidhi mipira 20 ya mwanzo kati ya 50 anayokusudia kuchangia katika ligi ya mpira wa miguu ya Bashungwa 2024. Picha na Eliud Henry