Keifo FM

“Kilichonileta kwenu ni upendo tu wanalusungo,nimekuja ili tulie pamoja na tuhuzunike pamoja”.

9 June 2026, 2:20 am

Pichani ni diwani wa viti maalumu Anna Mosses Mwamakula akiwa pamoja na wananchi wa kata ya Lusungo muda mfupi kabla ya kukabidhi ya kutoa mkono wa pole kwa wahanga wa mafuriko katika kata hiyo na James Mwakyembe

“Kilichonileta kwenu ni upendo tuu wanalusungo,nimekuja ili tulie pamoja na tuhuzunike pamoja”.

Na James Mwakyembe

Baada ya kadhia ya mafuriko yaliyoikumba kata ya Lusungo miezi miwili iliyopita diwani wa viti maalumu chama cha mapinduzi na mlezi wa kata ya Lusungo kupitia jumuiya ya wanawake wilaya ya Kyela Anna Mosses Mwamakula ametoa mkono wa pole kwa wananchi wa kata hiyo ikiwa ni sehemu ya kuungana nao katika janga hilo.
Akitoa pole hiyo ya mahindi,chumvi na sabuni mbele ya wananchi waliojitokeza Mwamakula amesema amesukumwa kutoa kidogo hicho kama sehemu ya pole yake kutokana na kadhia zilizowakumba pamoja na kumshukuru diwani wa kata hiyo kwa namna alivyoshirikiana naye kufanikisha jambo hilo.

Pichani ni Diwani wa viti maalumu Anna Mwamakula akizungumza na wananchi wa kata ya Lusungo wakati wa kakabidhi msaada wa chakula kwa wahanga wa mafuriko kata ya Lusungo

Wakitoa neno la shukrani mbele ya diwani huyo baada ya kupokea chakula hicho wananchi hao wamemuomba kuwapelekea kilio chao kwa serikali ya halmashauri ya wilaya ya Kyela juu ya kuwajengea kuta zilizobomolewa na mto Lufilyo na maji kuingia katika makazi yao na kusababisha nyumba kubomoka.

sauto ya wananchi kuhusu kujenga kuta 22

Pia wakaiomba serikali kupitia diwani huyo kuiagiza idara ya mazingira hapa halmashauri ya wilaya Kyela kutoa kibari cha kuwawinda na kuwavuna wanyama aina ya boka wanaotoka mto Lufilyo wanaovamia na kuharibu mazao yao hasa mpunga hali inayotishia kukosa chakula katika msimu huu wa mavuno.
Sauti ya wananchi kuhusu boko 33
Naye diwani wa kata hiyo Albert Mwaitenda amemshukuru diwani Anna Mosses Mwamakula kwa msaada huo wa chakula alioutoa kwa wanalusungo huku akiomba serikali na Ofisi ya mbunge jimbo la kyela kuona namna nyingine ya kuwafikia wananchi wake ili kuwanusuru na kadhia hiyo ya mafuriko pamoja na kuishauri serikali kuwafukuza boko katika makazi ya watu.

Sauti ya diwani kushukuru 44
Pichani wa wananchi wa kata ya Lusungo wilayani kyela wakiwa na diwani wa viti maalumu chama cha mapinduzi Anna Mwamakula

Msaada uliotolewa kwa wananchi wa kata ya Lusungo ni Mahindi debe kumi na sita,sabuni katoni mbili na chumvi kwa kaya kumi na sita zilizofika katika eneo hilo wakiongozwa na diwani mwenyeji wa kata hiyo na afisa mtendaji wake.