Keifo FM

Kyela:Serikali kumtua ndoo mwanamke Kyela

27 December 2023, 20:03

Pichani ni mfereji unaoandaliwa kutandaza mabomba ya maji kutoka Busokelo hadi wilayani Kyela Picha na Masoud Maulid

Jumla ya shilingi bilioni nne zimetolewa na serikali ya Tanzania kwa wananchi wilayani Kyela ili kukamilisha mradi wa ujenzi wa mtandao wa maji safi na salama kutoka halmashauri ya Busokelo.

Na Masoud Maulid

Wananchi wilayani Kyela wameanza kuwa na matumaini ya kupata maji safi na salama kutoka chanzo cha maji Mbambo hadi Kyela mjini baada ya ahadi za muda mrefu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari wananchi wa kata ya Ipande,Nkonkwa,Mwaya na Kyela mjini wamesema kutokana na jitihada zinazoendelea, za utandazaji wa mabomba kutoka  chanzo cha maji Mbambo halmashauri ya Busokelo hadi kufika kata ya Mwaya kijiji cha Malungo,ni hatua ambayo imeleta matumaini kwa wananchi kuondokana na kilio cha maji.

Sauti ya wananchi wilayani kyela wakipongeza serikali kwa jitihada za kuwapelekea maji wananchi

Kwa upande wake Kenethi Kalolo Mpingo mkazi wa kijiji cha Kapamisya amesema mpaka sasa hatua iliyofikia inaridhisha kwa kuwa ahadi za viongozi waliotangulia zilikuwa nyingi japo utekelezaji wake haukuonekana hasa kwenye swala la maji hivyo wameipongeza serikali ya Mama Samia na kumshukuru Mbunge wa jimbo la Kyela kwa kulipigania hadi kufikia hatua iliyopo kwa sasa

Sauti ya kenethi mwananchi kutoka hapa wilayani kyela akishukuru serikali
Pichani ni mabomba ya maji yakiandaliwa kuingiza kwenye mifereji tayari kuanza kupeleka maji

Nae Bupe Kabona mkazi wa kijiji cha Malungo wilaya ya Kyela amesema mbunge wa jimbo la Kyela Ally Mlaghila Jumbe Kinanasi katika kipindi cha kampeni za uchaguzi wa mwaka 2020   aliahidi kushughulikia changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wilaya Kyela ambapo  jitihada zake zinakwenda kuondoa adha ya wa wanawake kutembea umbali mrefu kuyafuata maji.

sauti ya Bupe ikipongeza mbunge wa Kyela kwa jitihada zake za kuishawishi serikali

Mradi wa maji kutoka Mbambo hadi Kyela mjini utakaoghalimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni nne utawanufaisha zaidi ya wananchi laki tatu wanaoishi ndani ya Mamlaka ya mji mdogo wa Kyela kwa kupata maji safi na salama.