Keifo FM

Jinsi teknolojia ya habari, inavyo weza kuinua uchumi kwenye vituo vya radio

12 September 2023, 10:58

Muwezeshaji Amua Rushita akiendelea kutoa Elimu ya Habari Mtandao kwa Wandishi wa habari Jijini Mbeya.Picha na Emmanuel Jotham

Wandishi wa habari nyanda za juu kusini,wametakiwa kutumia Radio mtandao ili kufikisha habari kwenye jamii.na kuweza kuwafikia wadau kutoka sehemu mbalimbali nje na ndani ya Tanzania pamoja na kujipambambanua katika masoko ili kuinua uchumi kwenye vyombo vyao vya habari

Na Mwandishi wetu Emmanuel Jotham

Wandishi wa habari nyanda za juu kusini,wametakiwa kutumia Radio mtandao ili kufikisha habari kwenye jamii,na kuweza kuwafikia wadau kutoka sehemu mbalimbali nje na ndani ya Tanzania

Kauli hiyo imetolewa na mwezeshaji wa mafunzo kutoka Mtandao wa  Radio jamii Tanzania(TADIO) Amua Rushita katika mafunzo yanayo endelea jijini mbeya yakihusisha Radio 9 wanachama kutoka mikao ya nyanda za Juu kisini.

Amesema endapo wandishi wa habari wataweza kutumia vizuri RAdio mtando kwenye Vituo vyao vya Radio wanaweza kuongeza uchumi kwenye Vituo kupitia matangazo mbalimbali watakayo yapata kupitia mtandao pamoja na kuziibua  habari ambazo hazipewi kipa umbele na vituo vya habari vikubwa vya kitaifa.

Sauti ya muwezeshaji Amua Rushita

Kwa upande wake Afisa miradi kutoka mtandao wa radio jamii tanzania TADIO SAUM BAKARI amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wandishi wa habari wanatumia teknolojia ili kuweza kupaza sauti ya habari zinazotokea kwenye  jamii yao inayo wazunguka.

endapo wandishi wa habari wataweza kutumia vizuri RAdio mtando kwenye Vituo vyao vya Radio wanaweza kuongeza uchumi kwenye Vituo

Sauti ya Saum Bakari afisa miradi Tadio

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo  Lusy Daud amesema kuwa mafunzo hayo yamekuwa na umuhimu mkubwa katika kuwaongezea uelewa wa kutumia mtandao kujitangaza na kutangaza vituo vyetu na katika kuhakikisha vituo vinajipambanua katika swala la masoko.

Sauti ya Lusy Dashud

Mtandao wa radio jamii Tanzania TADIO imekuwa ni kawaida kuwajengea uwezo wandishi wa habari Tanzania katika Nyanja mbalimbali ili kukuza ujuzi na mafanikio ya taarifa kwenye vituo vya Radiao .