Karagwe FM
Karagwe FM
3 March 2026, 8:11 pm

Wilaya ya Missenyi imekabidhi kadi za bima ya afya kwa wote kwa makundi maalum yaliyoandikishwa kupata bima hiyo bila malipo
Na Respicius John, Missenyi
Mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga amezindua rasmi zoezi la usajili na ugawaji wa vitambulisho vya bima ya afya kwa wote kwa makundi maalum huku akitoa wito kwa wananchi kujiunga kwa wingi na bima hiyo ili kupata matibabu kwa gharama nafuu
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua usajili na ugawaji wa vitambulisho vya bima ya afya kwa wote kwa makundi maalum waliopata bima hiyo bure amewataka wananchi kuchangamkia bima hiyo inayotolewa kwa shilingi 150,000/= kwa kaya ya watu sita

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya Missenyi Dk. Jamil Yahya amesema kuwa serikali imetenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya kuwezesha makundi maalum kupata bima ya afya kwa wote bila malipo
