Karagwe FM

CHAUMMA waahidi mazingira bora soko la Kashai

3 October 2025, 6:41 pm

Mgombea udiwani kata ya Kashai bw. Avitus Leopold kupitia CHAUMMA. Picha na Theophilida Felician

Mgombea udiwani anayedai kusukumwa na uchakavu wa miundombinu ya soko la Kashai na kwamba anaweza kutatua changamoto hizo kwa kuwa naye ni mhanga.

Na Theophilida Felician, Bukoba

Mgombea udiwani kata ya Kashai manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kupitia chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Bw. Avitus Leopord ameyataja malengo mahususi yaliyomsukuma kugombea nafasi hiyo ikiwemo ya kutatua changamoto kubwa ya uchakavu wa miundombinu ya soko la Kashai

Amesema hayo Oktoba 3 mwaka huu wakati wa mahojiano na Radio Karagwe akiwa sokoni humo na kusisitiza kuwa upatikanaji wa soko bora unahitaji uthubutu wa viongozi na ushirikiano wa wafanyabiashara

Mgombea udiwani kata ya Kashai bw. Avitus Leopold

Akiongelea vipaumbele atakavyotekeleza ikiwa wananchi watamchagua kwa nafasi ya udiwani bw. Leopold amesema kuwa atahakikisha anashirikiana na wananchi katika marekebisho ya barabara na kuwatetea maafisa usafirishaji juu ya kero zinazowakabili

Mgombea udiwani kata ya Kashai bw. Avitus Leopold akieleza vipaumbele vyake

Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara wa samaki katika soko hilo wamekiri kuwepo kwa changamoto na kuwaomba wagombea waliojitokeza kuomba nafasi kuhakikisha wanatatua changamoto hizo

Wamesema kuwa miongoni mwa kero kubwa katika soko hilo ni miundombinu mibovu inayowalazimisha baadhi yao kuhama sokoni hapo

Baadhi ya wafanyabiashara wakieleza changamoto za soko hilo