Karagwe FM

Wazee walia na huduma duni za afya Bukoba

2 October 2025, 3:15 pm

Mzee Maulid Rashidi Kambuga. Picha na Theophilida Felician

Wazee katika maeneo mbalimbali nchini wameitumia siku ya wazee duniani kupaza sauti zao kwa serikali wakilalamikia mambo kadha kubwa likitawala suala la huduma duni za afya

Na Theophilida Felician, Bukoba.

Tarehe 1 Oktoba kila mwaka ni siku ya wazee duniani ambapo wazee manispaa ya Bukoba wametumia siku hiyo kwa kutaja changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo kero ya ukosefu wa matibabu licha ya serikali kuanzisha mpango wa dirisha la wazee katika vituo vya kutolea huduma ya matibabu hususani hospitali, zahanati na vituo vya afya.

Wakizungumza na Radio Karagwe nyakati tofauti manispaa ya Bukoba mkoani Kagera akiwemo mzee Maulid Rashidi Kambuga wamesema kwamba huduma ya matibabu kwa wazee imekuwa shida hata wanapofika vituo vya kutolea matibabu bado ni changamoto kwao.

Mzee Maulid Rashidi Kambuga
Mzee Benadi Mutagwaba Pastory. Picha na Theophilida Felician

Mzee Eliasi Habibu Kateme naye mzee Benadi Mutagwaba Pastory wamefafanua kuwa wazee wamesahaulika katika huduma mbalimbali sababu kuu wakiitaja kutokuwa na jumuia maalumu ya wazee kama yalivyo makundi mengine jambo ambalo lingewasaidia kutatua changamoto zao.

Baadhi ya wazee wa manispaa ya Bukoba wakipaza sauti zao kuhusu kero mbalimbali
Mjumbe wa baraza la wazee mkoa wa Kagera mzee Haruna Idd. Picha na Theophilida Felician

Naye mjumbe wa baraza la wazee mkoa wa Kagera mzee Haruna Idd amesema kwamba hupokea kero nyingi kutoka kwa wazee wenzake wakilalamikia ukosefu wa huduma wanapofika vituo vya kutolea matibabu huku bibi Veronica Rwegi akiiomba serikali kuongeza jitihada katika eneo hilo la matibabu kwa wazee.

Baadhi ya wazee waliozungumzia kero mbalimbali

Hata hivyo mzee Haruna Iddy Ishengoma ametoa ushauri kwa serikali ukilenga wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalumu kuhusu namna bora ya kuratibu mipango mahususi itakayowasaidia.

Mmoja wa wazee walioshiriki maadhimisho ya siku ya wazee duniani katika manispaa ya Bukoba Bi Veronica Rwegi. Picha na Theophilida Felician