Karagwe FM

Serikali yatunuku cheti cha utambuzi kwa SHIWACHANDO

29 August 2025, 7:11 pm

Waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalum Dkt Doroth Gwajima (mwenye kilemba kichwani) baada ya kuwakabidhi cheti SHIWACHANDO. Picha na Theophilida Felician

Wanaume katika jamii wametakiwa kuripoti ukatili unaofanyika dhidi yao,yakiwemo matukio ya unyanyasaji sambamba na kupigwa na wenza wao majumbani.

Na Theophilida Felician

Shirika la wanaume wanaopitia changamoto kwenye ndoa SHIWACHANDO limeipongeza serikali chini ya wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalum kwa kuwatunuku cheti cha utambuzi na pongezi kutokana na majukumu yao ya kupinga ukatili dhidi ya wanaume wanaonyanyasika katika ndoa zao.

Amebainisha hayo mwenyekiti wa shirika hilo na Rais wa wanaume wanaopigwa na wanawake majumbani Ernest Josephat Komba wakati akizungumza na Redio Karagwe kwa njia ya simu kutokea makao makuu ya shirika yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Komba amesema shirika la SHIWACHANDO limekuwa likipambana kuwasaidia wananchi hususani wanaume kuyaripoti matukio ya ukatili wanaofanyiwa na wenza wao, matukio ambayo yameendelea kujitokeza katika jamii, hivyo serikali baada ya kuona na kutambua juhudi hizo tayari imewakabidhi cheti kama chachu ya kuongeza bidii ya uwajibikaji .

Mwenyekiti wa shirika la wanaume wanaopitia changamoto katika ndoa zao na Rais wa wanaume wanaopigwa na wanawake majumbani Ernest Josephat Komba