Karagwe FM

Sangoma wanaotumia viungo vya binadamu kukiona

10 July 2025, 8:00 pm

Katibu mkuu wa TAMESOT Lukas Joseph Mlipu, Picha na Theophilida Felician

Siku chache baada ya Jeshi la Polisi mkoani Kagera kuwashikilia wanaume wawili ambao ni Kelvin Piason Mdolon (42), mkazi wa Mnyiha na mganga wa kienyeji pamoja na Randani Seme Mlomo (64), mkazi wa Mnyamwanga ambaye ni mtumishi wa chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Vwawa wilayani Mbozi, mkoa wa Songwe kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu, chama cha waganga wa tiba asili TAMESOT kimekuja na tamko kuhusu tukio hilo.

Na Theophilida Felician, Dodoma

Chama cha waganga wa tiba asili nchini TAMESOT kimetoa waraka mahsusi kwa serikali kufuatia tukio la kukamatwa kwa watu wawili wakiwa na viungo vya binadamu hivi karibuni mkoani Kagera.

Waraka huo uliotolewa na katibu mkuu wa TAMESOT Lukas Joseph Mlipu kutoka makao makuu ya ofisi za chama hicho zilizopo Kibaigwa mkoani Dodoma umevitaka vyombo vya upelelezi kama TAKUKURU, Jeshi la polisi na usalama wa taifa kuunda timu ya kuchunguza mtandao mzima wa uhalifu.

Pia imependekezwa kufungwa kwa waganga wa jadi wanaobainika kufanya kazi kwa kutumia  viungo vya binadamu sambamba na jeshi la polisi kufanya msako kwa waganga wa jadi wasiokuwa na leseni za kuwaruhusu kufanya kazi ya tiba asilia.

Sambamba na hayo serikali imetakiwa kuwaunga mkono wenye taasisi zinazosimamia waganga zinazotoa elimu ya kuwajengea uwezo na uelewa waganga hao kwa lengo la kuwasaidia uelewa wa matumizi bora ya tiba asili.

WARAKA KWA SERIKALI NA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU:-
KUKAMATWA KWA MTU MKOANI KAGERA AKIWA NA VIUNGO
VINAVYODHANIWA NI VYA BINADAMU NA VIFAA VYA MATAMBIKO.

  1. UTANGULIZI
    TAMESOT TANZANIA ikiwa ni taasisi inayo jihusisha na Usimamizi na Utoaji
    Elimu Kwa Waganga wa tiba asili nchini na maadili ya tiba asili Kuelimisha
    jamii utofauti wa Waganga wa Jadi au Kienyeji Katika Tasnia yetu ya tiba
    asili hapa nchini Imesikitishwa na tukio la kukamatwa kwa mtu Mmoja
    mkoani Kagera akiwa na sehemu za siri za binadamu zilizokaushwa ambavyo
    ni mfupa wa taya, pembe za wanyama wa porini na viungo vingine
    vinavyodaiwa kutoka chumba cha maiti mkoani Songwe.
    Tukio hili linaibua maswali makubwa kuhusu usalama wa afya ya jamii,
    biashara ya viungo vya binadamu, ushirikina wa kisiasa na kiuchumi, na
    mtandao wa watu wanaokiuka haki za marehemu na maadili ya taifa.
  2. MALENGO YA WARAKA HUU
    i. Kuishauri Serikali na vyombo vya dola kuhusu udhibiti wa matukio ya
    namna hii.
    ii. Kuwataka viongozi wa kisiasa, vyombo vya sheria, na taasisi za tiba
    asilia na jamii kwa ujumla kulaani matukio ya matumizi ya viungo vya
    binadamu.
    iii. Kutoa uchambuzi wa kisheria, kijamii na kiimani kuhusu tukio hili.
  3. MAELEZO YA TUKIO KWA MUJIBU WA TAARIFA ZILIZOPO
    Mtu mmoja alikamatwa Kagera akiwa na:
     Sehemu za siri za binadamu zilizokaushwa
     Mfupa wa taya ya binadamu
     Pembe mbili za wanyama wa porini
     “Kondoo la mwanamke” – > mfuko wa uzazi,
    Anadai alivipata kutoka chumba cha maiti mkoani Songwe. Aidha, Mhudumu
    wa nyumba ya wageni aliweza kufahamu yaliyomo kwenye begi na kutoa
    taarifa, Jambo linaloibua maswali kuhusu usiri na mtandao wa ushiriki katika
    tukio.
    KIIMANI:-
  4. Imani potofu kuhusu mafanikio:
    Kuna dhana inayopenya miongoni mwa baadhi ya wanasiasa au
    wafanyabiashara kuwa viungo vya binadamu vinatoa nguvu ya kutawala,
    kupata ushindi katika chaguzi mbalimbali, kupata mali (Kipato Kikubwa)
    aidha kinga ya kisiasa.
    Tameso T Tunasema hii ni imani potofu, isiyo na uhalisia wala siyo Misingi ya
    tiba ya asili yenye maadili.
  5. Kuvunjwa kwa heshima ya marehemu:
    Katika imani za Tiba asili jadi Kienyeji , mwili wa marehemu unaheshimiwa.
    Aidha kuchukua viungo vya malehemu ni sawa na kufuru na matusi kwa
    Maadili ya Mizimu tunayoiamini waganga wa tiba asili na Watangulizi wetu
    waliotutangulia.
  6. Viongozi wa waganga wa Tiba asili, kienyeji / Jadi waadilifu:
    Tunatoa wito kwa waganga wa jadi, na Jamii kwa Ujumla, na viongozi wa
    Makundi yote ya kijamii kulaani na kujitenga na aina hii ya Vitendo vya
    kichawi na vya kishirikina kwa Jamii, na Tuendelee kukemea Hasa kipindi
    hiki Cha Kuelekea uchaguzi Mkuu 2025 ambapo Matukio haya hujitokeza kwa
    kuwa shirikisha Wana Siasa kwa kigezo Cha kuwapatia Madaraka.
    MADHARA KWA JAMII
  7. Kupotea kwa maadili ya kitaifa:
    Tukio hili linaonyesha namna gani baadhi ya watu wameacha maadili na
    kujiingiza kwenye njia za Mkato za utajili na madaraka kwa njia zisizo halali,
    na Kwa Imani ya TAMESO Tananzania, Inakinzana Kwa asilimia 100% na
    vitendo hivyo vya kikatili vinavyofanywa na matapeli hao, aidha tunaishauli
    serikali wanapotiwa nguvuni wapewe adhabu kali kwani ni wauwaji kama
    wauwaji wengine.
    Pia TAMESO Tanzania tunasema hizo ni mbinu za Wanaotumia mwamvuli wa
    Tiba asili – Makutimakalauzinga na sio waganaga halisi kama jamii inavyo
    amini.
  8. Athari kwa hofu ya raia:
    Matukio haya yanatishia amani, yanachochea hofu, na yanaharibu taswira ya
    Tasnia yetu ya Tiba asili hapa chini na Taswira ya waganga wa jadi kwa
    ujumla.
  9. Uwezekano wa mtandao mkubwa wa kihalifu:
    TAMESO TANANZANIA Tunaamini kuwa haiwezekani mtu mmoja aweze kuiba
    viungo vya binadamu bila ushirikiano wa watu wengine kuanzia kwenye
    manunuzi katika hospitali, usafirishaji ikiwemo na wahitaji waliosababisha
    kufanyika kwa jambo hili hivyo tunaishauli serikali hasa jeshi la polisi
    yanapotokea matukio kama haya liweze kufuatilia mtandao mzima ili utiwe
    nguvuni na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
    MAPENDEKEZO YA TAMESO TANANZANIA:
  10. UCHUNGUZI MAALUMU WA KSEKTA: (inter – agency taskforce):
  11. Vyombo vya upelelezi (TAKUKURU, Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa)
    waunde timu kuchunguza mtandao mzima wa uhalifu huu.
  12. Kufungwa kwa waganga wa jadi wanaotumia viungo vya binadamu:
  13. Jeshi la polis kufanya Msako kwa waganga wa Jadi , Kienyeji wasiokuwa na
    lesseni za kuwaruhusu kufanya kazi zao.
  14. Serikali iwaunge Mkono wenye Tasisi zinazowasimamia waganga wa tiba
    asili na zinazotoa Elimu ya kuwajengea uwezo na uelewa waganga wa tiba asili
    Jadi /Kienyeji ili kuepusha ufinyu wa elimu kwa tasnia hii ya tiba asili nchini
    na badala yake kuwa na uwelewa wa matumizi bora ya tiba asili hapa nchini.
    5 Mapitio ya Sheria Na. 23 ya Tiba Asili ya mwaka 2002:
    Sheria hii ifanyiwe marekebisho ili iwe na adhabu kali dhidi ya waganga
    wachafu wanaochanganya tiba na uhalifu wa viungo na pia ishilikishe
    waganga watiba asili wenye uhalisia katika vikao vya ngazi zote vya maamuzi
    ikiwa ni pamoja na kuwa na msemaji katika bunge letu la jamuhuri ya
    muungano wa Tanzania.
    KAMPENI YA ELIMU KWA UMMA:
    Tameso T Tuanzishe kampeni za kitaifa kuelimisha Waganga wa Jadi/ Kienyeji
    na jamii kwa ujumla kuwa hakuna mafanikio ya kweli yanayopatikana kwa
    njia za kishirikina.
    TAMESO T tunaomba serikali, mashirika au wadau wanaoguswa na Tasnia hii
    ya tiba asili, watoe ruzuku ili kuiwezesha Tameso T kufanikisha kampeni hii
    yenye tija na kukomesha imani za kishirikina zinazopelekea mauwaji kwa jamii
    isio kuwa na hatia hapa nchini.
    HITIMISHO
    Tunaomba Serikali na vyombo vya habari kuchukulia tukio hili kwa uzito wa
    kiusalama, kiimani na kimaadili. Wakati umefika wa kutenganisha waganga
    wa jadi wa kweli na Makutimakalauzinga wanaofanya jinai kwa kisingizio cha
    kutoa huduma za tiba asili, aidha tunaiyomba jamii kwa ujumla iyelewe kuwa
    mganga wa tiba asili anatumia dutu za mimea, wanyama na sio kutumia
    viungo vya binaadamu.
    TAMESO Tanzania Tupo tayari kushirikiana na Serikali yetu tukufu na taasisi
    zote ili kuhakikisha jamii inalindwa na heshima ya binadamu inalindwa Kwa
    Maslahi mapana ya nchi yetu na kulinda Heshima ya Tasnia yetu ya tiba asili
    nchini:
    Imetolewa na:
    Lukas Joseph Mlipu
    Katibu Mkuu TAMESO T
    S L P 130 – Kibaigwa
    Dodoma:
    Email tamesottz@gmail.com