Karagwe FM

DED Missenyi apiga stop wenyeviti wa vijiji na vitongoji kutumia mihuri

5 April 2025, 5:53 pm

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Bw. John Paulo Wanga. Picha na Respicius John

Kumekuwepo malalamiko ya muda mrefu ya wananchi kutozwa fedha na wenyeviti wa vijiji na vitongoji ili wawasainie nyaraka na kuwagongea mhuri wa serikali kote nchini

Na Respicius John, Missenyi Kagera

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi mkoa wa Kagera Bw. John Paulo Wanga amepiga marufuku matumizi ya mihuri ya wenyeviti wa vitongoji na vijiji kutumika katika nyaraka mbalimbali wanazosaini na badala yake itumike mihuri ya maafisa watendaji wa vijiji na kata

Wakili Wanga ametoa marufuku hiyo wakati wa mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa serikali za mitaa wilayani yakilenga kuongeza uwezo na ufanisi katika maeneo yao ya kazi
 

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Bw. John Paulo Wanga
Baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wilayani Missenyi wakifuatilia mafunzo ya uongozi. Picha na Respicius John

Nao baadhi ya wenyeviti wa vijiji na vitongoji wameunga mkono marufuku hiyo wakisema kuwa upigaji wa mihuri katika nyaraka kulikuwa kukiwachonganisha na wananchi

Baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wilayani Missenyi