Karagwe FM

Buhaya Tegeka watoa shilingi milioni 1.5 kwa watoto Missenyi

24 February 2025, 7:04 pm

Wanachama wa kikundi cha WhatsApp Buhaya Tegeka wilayani Missenyi wakiwa na zawadi kwa ajili ya watoto wa mazingira magumu. Picha na Respicius John

Kikundi cha mtandao wa WhatsApp kijulikanacho kama Buhaya Tegeka wilayani Missenyi mkoani Kagera kimetoa mfano wa kunufaisha jamii kuliko kujinufaisha chenyewe kwa kuchangia vitu kadhaa vya mahitaji ya watoto

Na,

Respicius John, Missenyi-Kagera

Kikundi cha mtandao wa Whatsapp cha Buhaya tegeka kimeadhimisha miaka minne ya kuanzishwa kwake kwa kutoa zawadi zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja na nusu kwa watoto wanaoishi katika mazingira Magumu wilayani Missenyi

Hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo imefanyika katika kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Magharibi mtaa wa Kashozi wilayani Missenyi kwa kugawa zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni 1.5 zimetolewa kwa watoto wanaolelewa na kituo cha mtoto na kijana ELCT Kashozi

Afisa ustawi wa jamii wa kituo cha huduma ya mtoto na kijana Bi Lidwina Kabisha

Makamu mwenyekiti wa kikundi hicho Moses Ignatio amesema kuwa kikundi cha Buhaya Tegeka wameamua kufanya matendo ya huruma wakati wakiadhimisha miaka mine tangu kianzishwe mtandaoni ambapo pia mmoja wa wanakikundi amesema kuwa tendo hilo ni kurudisha fadhila kwa jamii inayowazunguka

Makamu mwenyekiti wa Buhaya Tegeka Bw. Moses Ignatio pamoja na mmoja wa wanakikundi Bw. Jonex Kanshwi
Mwenyekiti wa uwakili kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Kashozi Mwalimu Julius Mulokozi. Picha na Respicius John

Mwenyekiti wa uwakili kanisani hapo Mwalimu Julius Mulokozi amewashukuru watu wa kikundi hicho na kutoa wito kwa vikundi vingine kuiga mfano wa kikundi hicho

Mwenyekiti wa uwakili kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Kashozi Mwalimu Julius Mulokozi
Baadhi ya wanakikundi wakigawa zawadi kwa watoto. Picha na Respicius John