Karagwe FM

CHADEMA Bukoba wadai kutowatambua viongozi serikali za mitaa

3 February 2025, 9:05 pm

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA jimbo la Bukoba mjini Bw. Chifu Karumna. Picha na Theophilida Felician

Baada ya mchakato wa uchaguzi ndani ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA ngazi ya taifa kukamilika na Tundu Lissu kuchaguliwa kuwa mwenyekiti, chama hicho kimeendelea na kazi ya kusimamia nidhamu ya wanachama mikoani na wilayani

Na Theophilida Felician, Bukoba

Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA jimbo la Bukoba  mjini kimetangaza msimamo wake wa kuungana na chama taifa kutowatambua viongozi wa serikali za mitaa waliochaguliwa mnamo Novemba 27, 2024.

Kupitia kwa mwenyekiti wa chama hicho jimbo hilo Chifu Karumna akiwahutubia wanachama  baada ya kupata taarifa ya taathimini ya uchaguzi kwenye mkutano mkuu maalumu uliofanyika katika kata ya Kashai manispaa ya Bukoba Chifu Karumna amewatangazia kwamba kuanzia sasa hawatawatambua wala kuwapa ushirikiano viongozi hao waliochaguliwa kupitia chama cha mapinduzi CCM.

Amesema  kuwa uchaguzi  uligubikwa na changamoto mbalimbali  ikiwemo ukandamizaji  dhidi yao kutoka kwa vyombo dola  hali iliyodhoofisha ushiriki wao katika kuwapata viongozi watokanao na CHADEMA na badala yake walishinda waliokuwa wagombea wa CCM mitaa yote ya jimbo hilo.

Sauti ya mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Bukoba mjini Chifu Karumna
Baadhi ya wanachama na viongozi wa CHADEMA jimbo la Bukoba mjini. Picha na Theophilida Felician

Hata hivyo mkutano huo imeazimia kuwavua uanachama waliokuwa wagombea wa nafasi ya uenyekiti baada ya kuthibitika kufanya usaliti na kujiondoa kwenye mchakato huo hatua ya mwisho kabla ya kufanyika uchaguzi

Sauti ya viongozi wa CHADEMA jimbo la Bukoba mjini