Karagwe FM

Kagera mguu sawa kupambana na marburg

29 January 2025, 10:39 pm

Mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwasa akizungumza na wanahabari wakati wa mafunzo kuhusu kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Marburg. Picha na Jovinus Ezekiel

Serikali ya mkoa wa Kagera imeahidi kuongeza juhudi za kudhibiti magonjwa ya hatari ukiwemo ugonjwa wa Marburg uliojitokeza kwa mara ya pili ndani ya kipindi kifupi tangu uripotiwe kwa mara ya kwanza mwaka 2023 na kudhibitiwa

Na Jovinus Ezekiel, Bukoba

Serikali mkoani Kagera imeahidi kuendeleza juhudi za kupambana na ugonjwa wa Marburg ulioripotiwa wilayani Biharamulo hivi karibuni.

Akizungumuza katika mafunzo ya siku moja iliyowakutanisha waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari mkoani Kagera Januari 28. 2025 kwa lengo la kuelimishwa namna ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa huo, mkuu wa mkoa wa Kagera Hajath Fatma Mwasa amesema kuwa waandishi wa habari wanayo nafasi kubwa ya kutumia vyombo vyao vya habari kutoa elimu kwa wananchi

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwasa akihutubia wanahabari
Baadhi ya wandishi wa habari walioshiriki wafunzo ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa Marburg mkoani Kagera wakiwa na mkuu wa mkoa wa Kagera na wadau wengine wa afya. Picha na Jovinus Ezekiel

Ameongeza kuwa mkoa wa Kagera utaendelea kuweka juhudi za kupambana na ugonjwa huo kwa kutumia wataalam wake wa idara ya afya huku akiwasisitiza wandishi wa habari kuisaidia jamii katika kupata taarifa sahihi za kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu na kudhibiti upotoshaji

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwasa

Kwa upande wake afisa afya wa mkoa wa Kagera Yassin Mwinori amesema kuwa kwa sasa mkoa wa Kagera umeweka vituo maalum vya kuwahifadhi wananchi watakaogundulika na ugonjwa huo hasa katika maeneo ya wilaya za mpakani.

Baadhi ya wandishi wa habari wakishiriki mafunzo kuhusu kupambana na maambukizi ya Marburg. Picha na Jovinus Ezekiel