Karagwe FM

DC Maiga aahidi kudhibiti uchomaji moto Missenyi

15 June 2024, 6:23 pm

Mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga akipanda mti wakati wa kampeni ya kudhibiti uchomaji moto katika misitu ya wilaya hiyo. Picha na Respicius John

Na Respicius John

Mkuu wa Wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamisi Mayamba Maiga amezindua kampeni ya kudhibiti vitendo vya uchomaji moto mazingira huku mwenyekiti wa halmashauri ya Missenyi Projestus Tegamaisho akiomba vyombo vya dola kutoa adhabu kali kwa wachoma moto.

Akizindua kampeni hiyo inayotekelezwa na wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) wilaya ya Missenyi inayolenga kudhibiti vitendo cha moto wilayani humo kanali mstaafu Maiga ameahidi kuunda kikosi kazi kwa ajili ya kubaini na kuchukua hatua wote wanaojihusisha na vitendo hivyo

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Missenyi kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Projestus Tegamaisho. Picha na Respicius John

Awali wakati akifungua mafunzo kwa wajumbe wa kamati ya maliasili kutoka katika ukanda wa tarafa ya ukanda wa Kiziba mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Projestus Tegamaisho ameiomba serikali kuchukua hatua dhidi ya watu watakaobainika wakijihusisha na uchomaji moto misitu

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Missenyi Projestus Tegamaisho
Meneja wa wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) wilaya ya Missenyi Mrisho Juma Athumani (aliyesimama). Picha na Respicius John

Kwa mujibu wa taarifa ya meneja wa TFS wilaya ya Missenyi Mrisho Juma Athumani tatizo la uchomaji moto misitu ni kubwa wilayani Missenyi ambapo baadhi ya wananchi walipewa mafunzo ya kudhibiti hali hiyo wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu kwa umma

Sauti ya meneja wa TFS wilaya ya Missenyi Mrisho Juma Athumani pamoja na baadhi ya wananchi