Karagwe FM

214 watunukiwa vyeti vya udereva kutoka VETA Kagera

11 June 2024, 1:05 pm

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya udereva wakiwa na viongozi wa chama na serikali wilaya ya Karagwe katika hafla ya kuwatunuku vyeti vya mafunzo ya udereva Juni 11, 2024. Picha na Ospicia Didace

Wimbi la madereva wa vyombo vya moto waisiokuwa na mafunzo wala leseni limeendelea kupungua nchini siku hadi siku kutokana na mikakati ya serikali na wadau wanaoratibu mafunzo ya jumla yanayotolewa kwa ufadhili wa taasisi au mashirika na kuwawezesha washiriki kupata mafunzo na leseni kwa muda mfupi na gharama nafuu.

Na Ospicia Diace

Mkuu wa wilaya ya Karagwe Julius Laiser  amefunga mafunzo ya madereva wa  magari na pikipiki  pamoja na kuwatunuku vyeti wahitimu 214 wa walioshiriki mafunzo hayo huku akiwataka kuzingatia yote waliyofundishwa ili kupunguza ajali za barabarani.

Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyoendeshwa na VETA Kagera kwa ufadhili wa chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Karagwe Laiser aliwataka madereva hao kuutumia ujuzi walioupata katika kuepusha ajali zisizo za lazima.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Karagwe Julius Laiser

Akiongea  wakati wa kufungwa kwa mafunzo hayo Mkurugenzi wa VETA Kagera Winston Kabantega na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Karagwe  bw. Paschal Rwamugata wamewaomba maderevaa hao kuwa mabalozi wazuri kwa madereva wengine.

Mkuu wa wilaya ya Karagwe Julius Laiser (aliyesimama), kushoto kwake ni Winstone Kabantega na kulia kwake ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya Karagwe Paschal Rwamugata. Picha na Ospicia Didace
Sauti ya mkurugenzi wa VETA Kagera Winstone Kabantega na mwenyekiti wa CCM Karagwe Paschal Rwamugata

Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wilayani Karagwe mkaguzi wa polisi Deusdedit Muguha amesema kuwa kuna sababu tatu za ajali ambapo ajali zinazotokana na mtu mwenyewe inaongoza kwa aslimia 76.

Sauti ya mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wa jeshi la polisi wilaya ya Karagwe mkaguzi wa polisi Deusdedith Muguha
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya udereva wakiwa ukumbini na kula kiapo cha kutii sheria za usalama barabarani. Picha na Ospicia Didace