Karagwe FM

Watoto kukosa chakula shuleni ni chanzo cha lishe duni Missenyi

11 June 2024, 12:14 pm

Afisa lishe wilaya ya Missenyi bi Faustina Godwin. Picha na Respicius John

Kumekuwa na changamoto kubwa ya lishe kwa watoto mkoani Kagera ambapo baadhi ya shule zilibuni mkakati wa kuwezesha wanafunzi kupata lishe shuleni. Hata hivyo baadhi ya wazazi hawaoni umuhimu wa kuchangia lishe ya watoto wao wawapo shuleni.

Na Respicius John

Uelewa mdogo kwa watoa huduma za afya ngazi ya jamii pamoja na utelekezaji wa watoto na familia vimetajwa kuwa kikwazo cha utoaji huduma za lishe wilayani Missenyi mkoani Kagera. Katika taarifa ya lishe kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2023/2024 iliyosomwa na afisa lishe bi Faustina Godwin kwa wajumbe wa kamati ya lishe wilaya ya Missenyi imebainisha baadhi ya changamoto huku akitaja baadhi ya shughuli zilizofanyika chini ya ofisi yake

Sauti ya afisa lishe wilaya ya Missenyi bi Faustina Godwin

Kwa upande wake afisa ustawi wa jamii wilaya ya Missenyi Evance Mvungi alitumia kikao hicho kuwataka akina mama wilayani humo kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya wakati wa ujauzito kupata elimu ya lishe kwa wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano

Sauti ya afisa ustawi wa jamii wilaya ya Missenyi Evance Mvungi
Afisa elimu taalumu wilaya ya Missenyi mwalimu Bita Maijo. Picha na Respicius John

Naye afisa elimu taaluma wilaya ya Missenyi mwalimu Maijo amesema kuwa idara ya elimu msingi inaendelea na juhudi za kuhakikisha wanafunzi wanapata lishe shuleni kwa wingi

Baadhi ya wajumbe wajumbe wa kamati ya lishe wilaya ya Missenyi. Picha na Respicius John