Karagwe FM

DC Maiga awapa matumaini ya ajira walimu wa shule binafsi Missenyi

31 May 2024, 6:38 pm

Mkuu wa wilaya ya Missenyi mkoani Kagera kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga (mwenye kofia) katika picha ya pamoja na watumishi wa shule ya awali na msingi ya kiingereza Bunazi Green Acres. Picha na Respicius John

Kumekuwa na kasumba kwamba walimu wanaofundisha katika shule binafsi hawawezi kupata ajira serikalini hali inayowafanya kukata tamaa na kubaki wakibembeleza ajira zao hata kama mazingira ya kazi ni magumu.

Na Respicius John

Mkuu wa wilaya ya Missenyi mkoani Kagera kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga amewataka walimu wa shule za msingi na sekondari wilayani humo kuendelea kujitolea katika maeneo wanakohudumu na kuongeza ubunifu zaidi katika masomo wanayofundisha ili kuwashawishi waajiri na wanafunzi kuwaamini.

Alisema hayo Mei 29, 2024 wakati wa ziara yake ya siku moja katika shule ya awali na msingi ya kiingereza Bunazi Green Acres iliyoko kata ya Kassambya alikokagua hali ya miundombinu ya shule hiyo na kuwasisitiza walimu kuongeza juhudi na bidii ili viwatangaze walimu hao katika soko la ajira hata serikalini.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Missenyi mkoani Kagera kanali mstaafu Hamis Mayamba Maiga
Meneja wa shule ya awali na msingi ya kiingereza Bunazi green acres bi Namala Tibanga (aliyesimama). Picha na Respicius John

Meneja wa shule ya awali na msingi ya kiingereza Bunazi green acres bi Namala Tibanga amemshukuru mkuu wa wilaya ya Missenyi kwa ushirikiano na shule hiyo na kumhakikishia kuwa uhusiano huo unafanywa pia na watumishi walioko chini ya ofisi ya mkuu wa wilaya wakisimamia sekta ya elimu na kwamba wanajivunia kufanya kazi wilayani Missenyi

Sauti ya meneja wa shule ya awali na msingi Bunazi green acres bi Namala Tibanga
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya awali na msingi Bunazi green acres iliyoko wilayani Missenyi mkoa wa Kagera wakiwa darasani. Picha na Respicius John