Zenj FM

Wakala wa ulinzi JKU fursa mpya ya mapato, ubunifu Zanzibar

5 January 2026, 8:18 pm

Waziri wa mawasiliano Teknolojia ya habari na ubunifu Mudrik Ramadhan Soraga wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ofisi ya wakala wa ulinzi JKU Mtoni.

Na Berema Nassor.

Waziri wa mawasiliano Teknolojia ya habari na ubunifu Mudrik Ramadhan Soraga amesema lengo na dhamira ya Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuanzisha taasisi ya wakala wa ulinzi JKU ni kuhakikisha serikali inapata mapato yatokanayo na huduma za ulinzi kutoka katika sekta ya utalii uwekezaji  na biashara.

Hayo ameyaeleza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ofisi ya wakala wa ulinzi Jku Mtoni amesema wakati umefika sasa  kwa wakala wa ulinzi JKU kuzidisha ubunifu na kujituma  zaidi ili kuweza kutoa huduma kwa serikali na taasisi binafsi kwa lengo la kupata mafanikio kwa maslahi ya taifa na jamii kwa ujumla.

Sauti ya Waziri wa mawasiliano Teknolojia ya habari na ubunifu Mudrik Ramadhan Soraga.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maluum za SMZ  Mikidadi Mbarouk Mzee amesema lengo la mradi huo ni miongoni mwa kuboresha mazingira bora na rafiki kwa watumishi wa wakala wa ulinzi JKU.

Sauti ya Naibu Katibu Mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maluum za SMZ  Mikidadi Mbarouk Mzee

Nae Mkuu wa Utawala wa JKU Zanzibar Kanal Haji Ali Ali  ameahidi kwamba ujenzi huo utakidhi viwango na ubora unaotakiwa  kwa lengo la kufanya kazi kwa bidii na weledi zaid.

Sauti ya Mkuu wa Utawala wa JKU Zanzibar Kanal Haji Ali Ali.

Uwekaji wa jiwe la msingi  la ofisi ya wakala wa Ulinzi Jku Mtoni ni miongoni mwa shamrashamra za maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi matukufu Zanzibar.