Zenj FM

ZAPONET kuimarisha uwezo wa wasaidizi wa sheria Zanzibar

15 December 2025, 4:02 pm

Viongozi wa ZAPONET wakiwa na viongozi wa Jumuya ya Wasaidizi wa Sheria wilaya ya Kaskazini B NOBPAO Mahonda mkoa wa Kaskazini unguja.

Na Mary Julius.

Mtandao wa Jumuiya za Wasaidizi wa Sheria Zanzibar, ZAPONET, umeanzishwa kwa lengo la kuzijengea uwezo taasisi zinazotoa huduma za msaada wa kisheria Unguja na Pemba ili ziweze kujisimamia na kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea Jumuiya za Wasaidizi wa Sheria katika wilaya za Magharibi A, Kaskazini B na Kaskazini A, Mshauri Elekezi wa ZAPONET, Asia A. Hussein, amesema mtandao huo unalenga kuimarisha uwezo wa taasisi hizo kiutendaji, kiuchumi na kitaaluma.

Aidha amesema changamoto zilizokuwa zikizikabili jumuiya hizo zilikuwa nyingi, hivyo ujio wa ZAPONET utasaidia kuhakikisha wanapata msaada wa kutosha na kujengewa uwezo wa kitaasisi ili kufikia malengo yao.

Sauti ya Mshauri Elekezi wa ZAPONET, Asia A. Hussein.

Kwa upande wake, Katibu wa ZAPONET Othuman Abass Othoman amesema lengo la ziara hiyo ni kuitambulisha rasmi ZAPONET kwa jumuiya za wasaidizi wa sheria, kuimarisha mashirikiano na kuhakikisha kila mwanachama anaielewa dhima ya mtandao huo.

.Sauti ya Katibu wa ZAPONET Othuman Abass Othoman.
Viongozi wa ZAPONET wakiwa na viongozi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria wilaya ya Magharib A

Naye Mratibu wa Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Magharibi A, PAUWA Safia B. Amran, amewahimiza wananchi kuzitumia jumuiya za wasaidizi wa sheria ili waweze kupata haki zao kwa urahisi, huku akiomba ushirikiano wa karibu kati ya ZAPONET na jumuiya hizo.

Sauti ya Mratibu wa Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Magharibi A, PAUWA Safia B. Amran,

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Kaskazini B, NOBPO Shaban Sarboko Makarani amesema ujio wa ZAPONET ni faraja kubwa kwani utaimarisha ubadilishanaji wa uzoefu, maarifa na mbinu za kutatua changamoto mbalimbali, pamoja na kusaidia upatikanaji wa rasilimali fedha.

Sauti ya Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Kaskazini B, NOBPO  Shaban Sarboko Makarani amesema ujio wa ZAPONET.
Viongozi wa ZAPONET wakiwa na viongozi wa Jumuiya ya Wasaidiazi wa Sheria wilaya ya Kaskazini A.

Ziara ya ZAPONET imehitimishwa Wilaya ya Kaskazini A, ambapo  Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria  Wilaya ya Kaskazini A   NAPAC Asia Fadhili Makame  amesema  kuanzishwa kwa mtandao huo kutapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto zinazozikabili jumuiya za wasaidizi wa sheria, huku wakitoa wito wa ushirikiano wa pamoja ili kufanikisha malengo ya kuanzishwa kwa mwamvuli huo.

Sauti ya Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria  Wilaya ya Kaskazini A   NAPAC Asia Fadhili Makame.