Zenj FM

SMZ kuongeza bajeti ya afya kwa wanaoishi na VVU

1 December 2025, 7:20 pm

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla akiwa na Viongozi wa Serikali, Watendaji kutoka Tasisi mbali mbali waliofika katika hafla ya Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idris Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

Na Mary Julius.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itahakikisha  inaongeza Bajeti katika kusimamia utoaji wa huduma za afya kwa watu wanao ishi na virusi vya ukimwi ili kuimarisha upatikanaji wa huduma hizo kwa uhakika hayo yamebainishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali itahakikisha Sheria na Sera zote zinazingatiwa na zinalindwa dhidi ya ubaguzi na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya unakuwa wa haki kwa wote bila ya ubaguzi.

Amesema Zanzibar imefanikiwa kupunguza maambulizi mapya ya maradhi ya kimwi kutoka watu 362 kwa mwaka 2020 hadi kufikia watu 211 waliopata maambukizi mapya kwa mwaka 2025 jambo lililosaidi kupunguza vifo vitokanavyo na maradhi hayo kutoka vifo 230 kwa mwaka 2020 hadi vifo 115 kwa mwaka 2025.

Aidha Hemed amewasihi wananchi kutowanyanyapa na kuwabagua watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi kwani kufanya hivyo ni kudhorotesha jitihada za Serikali  za kumaliza maambukizi mapya ya Ukimwi.

Sauti ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ukimwi Dkt. Ali Salim Ali amesema juhudi za kuzuia maambukizo ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto zimezidi kufanikiwa kwa  kuonesha maendeleo chanya ya maambukizo yaliyo chini ya asilimia mbili  ikiwa ni hatua ya kufikia lengo la  kumaliza maambukizo ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Aidha, katika  kuhakikisha usawa wa upatikanaji wa huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi hasa wanaume  ushirikiano katika jamii unazidi kuimarishwa ili kuondoa vikwazo vinavyowazuia  wanaume kupata huduma muhimu za matibabu ya VVU.

Akisoma risala ya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Zanzibar  Sara Abdi Mwita amesema kutokana na Mashirika wafadhili kusuasua katika kutoa misaada hasa kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wanaiomba Serikali kuliangalia suala la dawa za ARV kuwekwa katika bajeti ya serikali ili huduma hio iendelee kuwa endelevu kwa wagonjwa wa Ukimwi.