Zenj FM

Jamii yatakiwa kuunga mkono chanjo mpya ya polio

22 April 2025, 5:24 pm

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud akizungumza na Maafisa wa Kamati ya Ulinzi na Usalama  Mkoa, watendaji wa ofisi hiyo pamoja na viongozi wa idara ya chanjo na kinga kutoka wizara ya afya.

Na Mwandishi wetu.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud  ameitaka jamii  kupokea mabadiliko ya ongezeko la dozi  ya  chanjo ya polio  kwa watoto    ili kuwakinga na ugonjwa huo ambao husabaisha ulemavu au  kufariki dunia .

Ameyasema hayo Afisi ya Mkoa Tunguu wakati akizungumza na Maafisa wa Kamati ya Ulinzi na Usalama  Mkoa, watendaji wa ofisi hiyo pamoja na viongozi wa idara ya chanjo na kinga kutoka wizara ya afya  kwa lengo la  kutoa elimu  juu ya mabadiliko ya chanjo hiyo.

Amesema Tanzania ikiwemo Zanzibar  ni miongoni mwa Nchi ambazo  zimekua zikilipa umuhimu  suala chanjo kwa wananchi wake  hali ambayo imepelekea  kuiwezesha nchi  kuwa na idadi  ndogo ya watu wanaoathirika na magonjwa mbali mbali ikiwemo ugonjwa huo ukilinganisha na baadhi ya nchi nyengine ulimwenguni hivyo ni vyema kwa wazazi kupeleka watoto wao  wakati utakapowadia ili kuwakinga na mgonjwa.

Aidha amesema Serikali imekuwa makini na ina jali wananchi wake katika kuwakinga juu ya madhara ya magonjwa mbalimbali hivyo amewasisitiza  wananchi kuondokana na dhana potofu kuwa chanjo hizo zina madhara na mabadala yake kuunga mkono juhudi za serikali katika kutokomeza magonjwa hatarishi nchini.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud.  

Nae Mkurugenzi huduma za kinga Zanzibar kutoka Wizara ya Afya Dkt Salim Slim amesema lengo la Serikali kupitia Wizara ya afya ya kutoa chanzo hizo ni kutokomeza kabisa ugonjwa huo kwa jamii hasa kwa watoto.

Sauti ya Mkurugenzi huduma za kinga Zanzibar kutoka Wizara ya Afya Dkt Salim Slim.

Nao washiriki wa kikao hicho wameahidi kuieneza elimu hiyo kwa jamii ili kuona zoezi hilo linafanikiwa kama ilivyokusudiwa.

Sauti ya washiriki.

zoezi hilo la chanjo ya polio ya kutumia njia ya sindano linalotarajiwa kufanyika tarehe 1 mei litahusisha watoto kuanzia umri wa miezi tisa katika maeneo yote ya   unguja na pemba. mkoa