Zenj FM

Mpango mkakati wa miaka 5 uendane na uimarishaji huduma bora kwa jamii

8 October 2024, 4:40 pm

Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud, akizungumza na madiwani, viongozi kutoka benki ya NMB na PBZ pamoja na watendaji wa baraza hilo katika kikao cha mapitio ya  rasimu ya utaarishaji wa mpango mkakati  wa   miaka  mitano unaoanzia 2025/2030.

Na Mary Julius.

Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud, amewataka  viongozi na watendaji  wa baraza la mji kati Kuhakikisha  mpango mkakati wa miaka mitano wanao uandaa unalenga uimarishaji wa huduma  Bora  kwa jamii na unakidhi  mahitaji  ya wananchi.

Ayoub ameyaeleza hayo huko Dunga ukumbi wa baraza la mji kati wakati akizungumza na madiwani, viongozi kutoka benki ya NMB na PBZ pamoja na watendaji wa baraza hilo katika kikao cha mapitio ya  rasimu ya utaarishaji wa mpango mkakati  wa   miaka  mitano unaoanzia 2025/2030.

Amesema watendaji wanapaswa kutambua kwamba  ili mpango huo unaoandaliwa uweze  kutekelezekaipasavyo unahitaji kupata maoni ya wananchi kulingana na wakati  wa sasa na wa baadae pamoja   na usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato na utunzaji wa raslimali kwani nchi nyingi duniani  mabaraza na manispaa yameweza kupiga hatua kubwa za maendeleo kutokana na utaratibu huo 

Aidha amewasisitiza  watendaji hao kuendelea kuongeza kasi ya uwajibikaji ili kuliongezea hadhi baraza hilo liweze kupanda kutoka baraza la mji Kwenda manispaaa.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja  Ayoub Mohd Mahmoud,

Mkurugenzi wa Baraza la mji kati  Salum Mohd AbubKar amesema mpango huo wa miaka mitano umelenga  kushirikisha  jamii katika nyanja mbali mbali za kiuchumi ikiwemo  utunzaji wa rasimali, uchumi Wa bluu, usafi wa mazingira, pamoja  na kuweka mipango miji ilio Bora.

Sauti ya Mkurugenzi wa Baraza la mji kati  Salum Mohd AbubKar.

Kwa upande wake Mshauri Elekezi  kutoka Dar-es-saalam Dk Pauline Mtunda amesema kutokana na mpango huo ni vyema kwa Baraza hilo kuwa na mipango madhubuti ya ukusanyaji na matumizi ya mapato yatokanayo kodi za wananchi kuona zinarudi kuwanufaisha  kupitia  miradi ya maendeleo.

Sauti ya Mshauri Elekezi  kutoka Dar-es-saalam Dk Pauline Mtunda.